• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi atoa siku saba Afisa Ardhi aliyehamishwa arudishwe Rorya

Posted on: May 31st, 2024

Mkuu wa Mkoa leo amefanya ziara katika Halmashauri ya Rorya na kuzungumza na wafanyakazi wa Halmashauri hiyo ambapo ametoa siku saba kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kumrejesha Bwana Fred Kijalawa Afisa Ardhi Mteule aliyehamishiwa Wilaya ya Serengeti kujibu hoja Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kumuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia kumrejesha Bwana Kijalawa ili aisaidie Halmashauri kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusiana na fedha hizo.                

“DAS wasiliana na RAS mhakikishe huyu jamaa anarudi na anajibu hoja zote za ukaguzi kuhusiana na mradi huo ambao uliletewa fedha na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ndani ya siku saba” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mhe. Gerald Ng’ong’a ameeleza kuwa Halmashauri hiyo haipati ushirikiano wanaohitaji kutoka Idara ya Ardhi Wilaya ya Rorya ambayo imekuwa ikitekeleza miradi lakini haitoi taarifa kwenye Baraza la Madiwani.

Mhe. Ng’ong’a ameeleza kuwa Idara hiyo ilipewa fedha za mkopo shilingi bilioni moja ambapo mpaka sasa hamna taarifa ya matumizi ya fedha hizo na kuna hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambazo hazina majibu kutokana na kukosa taarifa.

“Kwa niaba ya Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Rorya tunaomba utusaidie kwa kumrejesha Afisa Ardhi aliyehusika na matumizi ya fedha hizo ambaye baada ya hapo alihamishiwa Wilaa ya Serengeti na hatoi ushirikiano katika kujibu hoja tulizonazo” amesema Mhe. Ng’ong’a.

Mhe. Ng’ong’a ameeleza kuwa waliwahi kumuomba KamishnaMsaidizi wa Ardhi Mkoa wa Mara kusaidia kujibu hoja hizo lakini mpaka sasa hoja zipo na Halmashauri haina majibu ya kuridhisha kuhusiana na matumizi ya fedha hizo katika utekelezaji wa mradi huo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, kwa sasa Idara hiyo imepewa miradi mingine miwili na Baraza la Madiwani halijui gharama za mradi, wanufaika wa mradi, mradi utatekelezwa eneo gani na unamanufaa gani na kumekuwa hakuna ushirikishwaji katika utekelezaji wa miradi hiyo.

“Sisi kama Halmashauri tunataka tupate taarifa ya miradi yote ambayo inatekelezwa na Wizara au taasisi nyingine za umma katika Halmashauri yetu ili tuweze kuijua na kuisimamia miradi hiyo kwa manufaa ya wananchi” amesema Mhe. Ng’ong’a.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Juma Chikoka ameeleza kuwa Wilaya inaendelea kuwahamasisha wananchi kutunza mifugo yao kwa kujenga mazizi ya pamoja ili kudhibiti wizi wa mifugo katika Wilaya hiyo.

Mhe. Chikoka amewataka wananchi kuipa hadhi inayostahili mifugo yao ili kudhibiti wimbi wa wizi wa mifugo katika wilaya hiyo. 

Mhe. Chikoka ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya imeanza kukawakaribisha uwekezaji katika ufuvi na ufugaji wa samaki wa kisasa kwa njia ya visimba na kuongeza kuwa kwa sasa kuna visimba 72 vya wadau na vya Serikali katika Halmashauri hiyo. 

Mhe. Chikoka amesema kwa sasa Serikali inatekeleza Mradi wa Maji wa Rorya-Tarime ambapo serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 134 katika mradi huo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa