• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ateta na TIC kuhusu uwekezaji Mkoa wa Mara

Posted on: July 22nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo amewapokea na kuzungumza na Maafisa kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) waliopo katika ziara ya kikazi Mkoa wa Mara na kuwataka kuwahamasisha wawekezaji zaidi kuwekeza katika Mkoa wa Mara.  

Akizungumza na maafisa hao, Mhe. Mtambi amesema Mkoa wa Mara una fursa nyingi za uwekezaji ikiwemo madini, uvuvi, ufugaji na utalii na kuitaka TIC kuwaleta wawekezaji zaidi katika maeneo hayo ili kuchangamkia fursa zilizopo.

“Mkoa wa Mara una malighafi na mazao mbalimbali hata hivyo hauna viwanda vya kutosha kuchakata alighafi hizo kuwa bidhaa na hivyo Mkoa unakosa faida za kiuchumi zinazotokana na malighafi hizo kuchakatwa ili uongezwa thamani” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kwa sasa mazingira yanaruhusu kwa uwekezaji na miundombinu imeboreshwa kwa ujenzi wa barabara, madaraja na vivuko na upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Musoma.

Mhe. Mtambi amesema Mkoa wa Mara umebarikiwa kuwa na zaidi ya asilimia 70 ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Ziwa Victoria na madini katika kila Wilaya ya Mkoa wa Mara lakini fursa hizi bado zinahitaji uwekezaji zaidi ili nchi iweze kupata manufaa makubwa ya kiuchumi.

Kanali Mtambi amewahamasisha wawekezaji mbalimbali kuwekeza katika Mkoa wa Mara na kuwaahidi kuwa kwa kufanya hivyo uwekezaji huo utawalipa mara dufu kwa kuna mahitaji makubwa ya wawekezji kutokana na fursa za uwekezaji zilizopo.

Ameyataja maeneo yaliyobainishwa kwa ajili ya uwekezaji kuwa ni pamoja na Bonde ya Bugwema lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Bonde la Mto Mara ambayo yanafaa kwa kilimo cha mazao ya chakula na biashara.

Kwa upande wake, Meneja wa TIC Kanda ya Ziwa Bi. Fina Jerome amesema Kituo cha Uwekezaji Tanzania kipo katika awamu ya pili ya kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani kwa kutumia fursa zilizopo nchini.

“Kwa awamu ya kwanza tumeshafika mikoa 17, kwa hii awamu ya pili tunataka kutembelea mikoa iliyosalia kuhamasisha fursa zilizopo katika mikoa hiyo ili zitumike kuinua uchumi wa mikoa hiyo na Taifa kwa ujumla” amesema Bi. Jerome.

Bi. Jerome amesema kupitia kampeni hiyo, TIC inalengo pia la kuangalia changamoto na mazingira ya uwekezaji kwa wawekezaji waliopo ili kutafuta namna ya kuzitatua ili kuwavutia wawekezaji wengi zaidi.  

Maafisa wa TIC wapo katika Mkoa wa Mara kwa ajili ya kampeni ya uwekezaji wa ndani awamu ya pili ambapo kesho tarehe 23 Julai, 2024 maafisa hao wataendesha semina ya kwanza ya uwekezaji kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara katika ukumbi wa uwekezaji.

 Kwa leo, mbali na kuwasili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kutia saini kitabu cha wageni, Maafisa hao wametembelea Wilaya ya Tarime kujionea uzalishaji katika baadhi ya viwanda na migodi ya kati iliyopo katika Wilaya hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa