• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ataka uwekezaji zaidi Ziwa Victoria

Posted on: May 31st, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo amezungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya na kuitaka Halmashauri hiyo kuongeza uwekezaji katika Ziwa Victoria ili kupanua wigo wa mapato ya Halmashauri hiyo yanayotokana na kuwepo kwa sehemu kubwa ya Ziwa Victoria.

Mhe. Mtambi ameeleza kuwa kwa sasa Halmashauri hiyo inapata mapato yanayotokana na shughuli za uvuvi wa samaki tu na kuitaka Halmashauri kusafisha fukwe za Ziwa Victoria na kuvutia wawekezaji katika ugufaji wa kisasa wa samaki, uwekezaji kwenye fukwe, shughuli za usafirishaji katika Ziwa Victoria na ujenzi wa viwanda vya kuchakata samaki, nyama na mazao.

“Kukiwa na boti za kisasa na usafiri mzuri katika Ziwa Victoria itakuwa rahisi kwa watalii baada ya kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kutalii pia katika Ziwa Victoria jambo ambalo litakuza uchumi wa Mkoa na mwananchi mmoja mmoja” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi ameeleza kuwa usafiri mzuri katika Ziwa Victoria utapanua uwekezaji wa hoteli za kisasa kandokando ya ziwa na kuongeza ajira kwa wananchi wa Wilaya ya Rorya na kuimarisha masoko ya wakulima, wafugaji na wavuvi baada ya watalii kuongezeka. 

Mhe. Mtambi ameeleza kuwa Wilaya hiyo ina eneo lenye mita za mraba 9,345 ambapo asilimia 77 ya eneo hilo ni Ziwa Victoria wakati Halmashauri inapata mapato kidogo yanayotokana na Ziwa Victoria kwa sababu hamna uwekezaji uliofanyika katika Ziwa na fukwe za Ziwa hilo .

“Tuweke mipango na mikakati inayoendana na jiografia ya eneo la Wilaya ya Rorya ili tutumie vizuri jiongrafia hiyo kupanua vyanzo vya mapato  ili kupata maendeleo endelevu ya Wilaya ya Rorya” Amesema Mhe. Mtambi.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kwa kufanikiwa kukusanya shilingi 1,535,618,289 hadi kufikia tarehe 27 Mei, 2024 ambayo ni sawa na asilimia 97 ya makusanyo ya mapato ya ndani yaliyopangwa kukusanya ya shilingi 1,590,456,000 katika mwaka wa fedha 2023/2024. 

“Baada ya kufanya uwekezaji katika Ziwa Victoria mapato ya wilaya hii yatakuwa endelevu kutokana na kuongezeka kwa biashara za mpakani kati ya Tanzania, Kenya na Uganda pindi usafiri wa majini ukiwa umeimarika” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mhe. Gerald Ng’ong’a ameeleza kuwa Baraza la Madiwani linaendelea kuisimamia Halmashauri na kufanikisha kupandisha makusanyo ya mapato ambapo hadi tarehe 27 Mei, 2024 Halmashauri imefanikiwa kukusanya shilingi 1,535,618,289.

Mhe. Ng’ong’a ameeleza kuwa Halmashauri katika mwaka wa fedha 2023/2024 ilipanga kukusanya shilingi 1,590,456,000 ambapo makusanyo mpaka sasa ni sawa na asilimia 97 ya makusanyo yote ya mwaka huu.

Mhe. Ng’ong’a ameeleza kuwa Halmashauri hiyo inategemea kuongeza zaidi mapato ya ndani baada ya kuwekeza katika ujenzi wa stendi katika eneo la Mika na matarajio stendi hiyo ikianza kutumika mapato yataongezeka.

Mwenyekiti huyo wa Halmashauri amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Madiwani na wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya jambo ambalo amesema linafanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi pamoja na Halmashauri hiyo kupata hati safi ya ukaguzi kwa miaka mitatu mfululizo.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Rorya Bwana Michael Bundala amewapongeza wafanyakazi kwa kazi nzuri wanazozifanya na kuiwezesha Halmashauri kupata hati safi ya ukaguzi.

Mhe. Bundala ameipongeza Halmashauri kuhusu ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuitaka Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kukumbuka kurejesha asilimia ya makusanyo yake kutekeleza miradi ya maendeleo katika vijiji.

Mhe. Bundala amewataka wataalamu wa Halmashauri kuwaandaa wananchi wa Wilaya ya Rorya kuchangamkia fursa za miikopo ya asilimia 10 kwa ajili ya vikundi vya akina mama, watu wenye ulemavu na vijana itakapoanza kutolewa Julai, 2024.

Mhe. Bundala amewataka viongozi na wataalamu wa Wilaya ya Rorya kutimiza wajibu wao na kuwahudumia wananchi na kutatua kero zao.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa