• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ataka msako wanafunzi ambao hawajaripoti shule

Posted on: March 5th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo tarehe 5 Machi, 2025 ameongoza kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji na kuwataka Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara kufanya msako wa kuwatafuta na kuwachukulia hatua wafafunzi wa kidato cha kwanza ambao hawajaripoti shule.

“Wakuu wa Wilaya anzeni msako katika maeneo yenu kuwatafuta hawa wanafunzi ambao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza na mpaka sasa hawajasajiriwa na kuhakikisha wote wanasajiriwa na kuanza masomo mapema iwezekanavyo” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa kuwa ni asilimia 82.3 tu ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ndio wamejisajiri mpaka tarehe 04 Machi, 2025 jambo ambalo amesema halikubaliki.

Mhe. Mtambi amesema hadi tarehe 04 Machi, 2025 wanafunzi wa awali waliosajiriwa walikuwa ni asilimia 99.61 huku waliosajiliwa darasa la kwanza walikuwa wamefikia asilimia 107 huku wanafunzi wa kuanza kidato cha kwanza wakiwa asilimia 82.3 tu ya wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga.

Mhe. Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya kuwakamata wazazi wote ambao watoto wao hawajaripoti shuleni na kuwachukulia hatua za kisheria na kuongeza kuwa kuna taarifa watoto hawa hawajaripoti shuleni kwa sababu wanajihusisha na uchimbaji wa madini, kuolewa na wengine ni uzembe tu wa wazazi.

Mhe. Mtambi amesema Serikali imewekeza fedha nyingi sana kujenga shule na kuboresha mazingira ya kujifunza na kufundishia lakini haitakuwa na faida inayotarajiwa kama watoto hawatapelekwa shule kujifunza.

“Mkoa wa Mara hautamfumbia macho mzazi yoyote atakayemkosesha mtoto kupata haki yake ya masomo” amesema Mhe. Mtambi na kukihakikishia kikao hicho kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wazazi wote wanaozembea kuwapeleka watoto shule.

Mhe. Mtambi pia amezitaka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuwasilisha mpango na bajeti ya  ukarabati wa shule chakavu zilizopo kwenye maeneo yao mwishoni mwa Aprili, 2025 na kuwataka wabunge kuwasilisha orodha ya shule chakavu zilizopo kwenye majimbo yao ili aweze kuziangalia orodha zote mbili na kujiridhisha.  

Aidha, amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula mashuleni ili waweze kujifunza vizuri na kuboresha ufaulu.  

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara Mhe. Ghati Zephania Chomete amesema suala la chakula mashuleni kutokana na umuhimu wake, Mkoa uwekeze kwenye kutoa elimu kwa wananchi ili wapate uelewa kuhusu umuhimu wa wao kuchangia.

“Tunatakiwa kuwaelimisha kuhusu tafiti za kitaalamu zilizofanyika kuhusu wanafunzi wanaokula shuleni wanavyofaulu ukilinganisha na wanafunzi ambao hawali chakula shuleni” amesema Mhe. Chomete.

Aidha, Mhe. Chomete amewataka wasimamizi wa Elimu kuhakikisha kuwa shule ambazo zina maeneo makubwa au mashamba zipewe maelekezo ili mashamba hayo yaweze kulimwa kwa ajili ya chakula cha wanafunzi.  

Kwa upande wake, Katibu wa Kamati ya Maridhiano na Amani ya Mkoa wa Mara Shehe Juma Masiroli amesema yeye ni mhamasishaji wa chakula mashuleni katika Mkoa wa Mara, ametembelea shule nyingi katika Manispaa ya Musoma sio shule nyingi zinatoa chakula shuleni kwa wanafunzi wote.

“Ni shule tatu tu za Serikali katika Manispaa ya Musoma ndio zinazotoa chakula kwa wanafunzi wote kwa asilimia 100 huku shule nyingi zinatoa kwa wanafunzi wachache wanaochangia” amesema shehe Masiroli.

Shehe Masiroli ametoa sababu mbalimbali zinazochangia ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanafunzi kuwapotosha wazazi kuwa chakula kinaliwa na walimu, umaskini miungoni mwa wazazi na walezi, siasa katika baadhi ya maeneo zinaathiri michango.

Bwana Masiroli ameishauri Serikali kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili wahamasike kutoa chakula mashuleni na wanafunzi waweze kusoma vizuri na wanafunzi wengine hata majumbani wakirudi hawana uhakika wa kupata chakula na hivyo kuwalazimisha kulala njaa wakiwa wameshinda na njaa.

Jumla ya wanafunzi 46,671 ambao ni sawa na asilimia 17.7 ya wanafunzi waliopangiwa kujiunga na kidato cha kwanza katika Mkoa wa Mara hawajaripoti shule kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uzembe wa wazazi, uchimbaji wa madini na ajira za watoto.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa