• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

Posted on: July 25th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amekabidhi Kompyuta 142 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya mawasiliano katika Zahanati, amewataka wasimamizi wa Sekta ya Afya kuhakikisha matumizi ya Mfumo wa GOTHOMIS unafika asilimia 100 katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika Hafla hiyo, Mhe. Mtambi amesema awali, Mkoa wa Mara ulikuwa unashika nafasi ya kwanza katika ufungaji na matumizi ya mfumo huo katika vituo vya kutolea huduma za afya na kwa sasa umeshuka baada ya mikoa mingine kuongeza jitihada.

“Sasa mhakikishe tunarudi kwenye nafasi yetu ya awali, na hii inawezekana baada ya kupata msaada huu ambao unaenda kutatua changamoto ya ukosekanaji wa vifaa katika vituo vya kutolea huduma za afya” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kwa sasa Mkoa hauna sababu ya kuendelea kubaki na matumizi ya mfumo wa GOTHOMIS kwa asilimia 90 na kuitaka Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kuhakikisha kuwa vituo vyote vya kutolea huduma za afya vinafunga na kutumia mfumo huo.

Aidha, Mhe. Mtambi ametoa hadi tarehe 30 Agosti, 2025 vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara viwe vimefungwa mfumo wa GOTHOMIS na kuzitaka Divisheni za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii vya Halmashauri kusimamia matumizi sahihi ya vifaa vilivyotolewa.

Kanali Mtambi amekemea tabia ya watumishi wa sekta ya afya kuchelewesha kutoa huduma kwa wananchi kwa kisingizio kuwa mfumo unasumbua ili watoe huduma nje ya mfumo jambo ambalo amesema linasababisha wizi wa fedha za Serikali.

“Watumishi ambao hawaujui vizuri mfumo au matumizi ya kompyuta wajifunze na kufanya mazoezi ya mara kwa mara ili kuboresha utendaji wao na kutoa huduma bora kwa wananchi bila visingizio” amesema Mhe. Mtambi.  

Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Ndugu Gerald Musabila Kusaya amesema vifaa hivyo vitausaidia Mkoa wa Mara katika kuimarisha matumizi ya mfumo wa GOTHOMIS ambao unaenda kudhibiti mapato ya Serikali katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, Ndugu Kusaya amesema matumizi ya mfumo yakiimarisha yatawezesha pia mawasiliano kuboreshwa kati ya vituo vya kutolea huduma za afya na taasisi mbalimbali za Serikali.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu ameishukuru Wizara ya Afya kwa kutoa Kompyuta hizo kwa Mkoa wa Mara na kuahidi kuzitumia kwa ajili ya kuboresha huduma za afya.

“Vifaa hivi vitasaidia kuboresha upatikanaji wa vifaa katika matumizi ya mifumo mbalimbali ya afya ili kutuwezesha kudhibiti mapato ya Serikali na utoaji wa taarifa kwa wakati” amesema Dkt. Masatu.

Halfa hiyo imehudhuriwa na Wakuu wa Sehemu na Vitengo vya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Kaimu Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Mara, Wakuu wa Divisheni za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • Mtambi aitaka FEZA kuwekeza Butiama kumuenzi Mwalimu Nyerere

    July 25, 2025
  • Mtambi amtaka mkandarasi mradi wa maji Rorya/Tarime kufanyakazi usiku na mchana

    July 22, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa