• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi Ataka Mabadiliko Sekta ya Uvuvi

Posted on: July 16th, 2024

MTAMBI ATAKA MABADILIKO KUTOKA KWA WAVUVI

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amefanya kikao na wavuvi wa Mkoa wa Mara katika ukumbi wa uwekezaji na kuwataka viongozi wa vyama vya uvuvi katika Mkoa wa Mara kuwaongoza wavuvi na kuleta mabadiliko chanya kwa wanachama wao.

Mhe. Mtambi amesema hayo wakati wa kuhitimisha kikao hicho na kuwataka makundi yote ya wavuvi kuungana na kuchagua uongozi wa wavuvi ukijumuisha viongozi wa makundi yote ndani ya siku saba ili kuimarisha Umoja wa Wavuvi wa Mkoa wa Mara.

“Ukiwa kiongozi unatakiwa kuonyesha mfano na kuonyesha njia ya kufikia maendeleo na kutatua  changamoto zinazowakabili kama wavuvi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo” amesema Mhe. Mtambi.

Amewataka viongozi wa wavuvi kuanzisha operesheni ya kudhibiti uvuvi haramu katika maeneo yao na kuwasimamia wavuvi waliochini yao ili waweze kuvua kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi na kuacha kulindana wao kwa wao wanapokuwa wamekiuka sheria na taratibu.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi na wavuvi kutoa taarifa pale wanapohisi wanakwama au wanakwamishwa kutekeleza majukumu yao au wanapowabaini wavuvi haramu ambao wanashindwa kuwadhibiti katika maeneo yao.

Mhe. Mtambi amewataka vongozi na watendaji wa Serikali kuhakikisha kuwa Kamati za Usimamizi za Rasilimali za Uvuvi (BMU) zinatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kanuni na kuwataka wanasiasa kuacha kuingilia utendaji wa kamati hizo katika maeneo yao.

Mhe. Mtambi amesema eneo la Mkoa wa Mara asilimia 36 ni Ziwa Victoria lakini mapato yanayotokana na Ziwa hilo yanahusisha uvuvi peke yake na kwa kiasi kikubwa Mkoa haufaidi eneo hilo kutokana na uvuvi haramu unaoendelea kwa kiasi kikubwa.

Mhe. Mtambi ameagiza kuteketezwa kwa nyavu zote zilizokamatwa zilizopo katika bohari siku ya Ijumaa tarehe 19 Julai, 2024 na kuwataka  viongozi wa vyama vya wavuvi kusaidia kuteketeza nyavu haramu wanazokamata katika maeneo yao.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa Bwana Gerald Musabila Kusaya amesema Mkoa wa Mara una eneo lenye kilomita za mraba 10,854 za maji ya Ziwa Victoria ambayo ni sawa na asilimia 36 ya eneo lote.

Bwana Kusaya amesema Mkoa una mialo ya uvuvi 151 na kati ya hiyo 127 ni mialo rasmi huku mialo 24 ikiwa sio rasmi lakini inatumiwa na wavuvi wa Mkoa wa Mara wapatao 17,093 wanaofanya shughuli zao katika Ziwa Victoria na Mto Mara.  

Bwana Kusaya amesema, Mkoa wa Mara una wavuvi wengi na watu ambao wanahusika na mnyororo wa uvuvi ikiwemo wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi ambao ni wengi na wote maisha yao yanategemea kukua kwa sekta ya uvuvi.

Amesema kwa sasa Serikali imeboresha mazingira katika sekta ya uvuvi ikiwemo na utoaji wa mikopo ya wavuvi na wafugaji wa samaki kwa riba nafuu kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) ambapo tayari baadhi ya wavuvi wa Mkoa wa Mara wamenufaika na mikopo hiyo.

Kwa upande wake,mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Omari Gamuya  amesema katika maeneo ya wavuvi kuna takriban kaya 96,097 ambazo hazina vyoo bora na kuwahamasisha wavuvi kujenga na kutumia vyoo bora katika maeneo yao na mialo ya uvuvi ili kupunguza uwezekano wa kutokea kwa magonjwaya mlipuko.

Dkt. Gamuya amesema katika mialo, kambi za wavuvi na maeneo yao ya makazi kwa sehemu kubwa hayana vyoo bora na hivyo wengi wao hawatumii vyoo katika kujisaidia jambo ambalo ni hatarishi kwa maisha ya watu katika maeneo hayo.

 Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wakurugenzi wa Halmashauri na Wataalamu wa Uvuvi kutoka Halmashauri saba za Mkoa wa Mara zinazojihusisha na uvuvi ambazo ni Musoma Manispaa, Musoma DC, Bunda DC, Butiama DC, Bunda TC, Rorya na Tarime DC.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa