• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi asikiliza kero za wananchi

Posted on: July 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi katika utaratibu wake wa kawaida wa kusikiliza kero za wananchi siku ya Ijumaa, leo tarehe 5 Julai, 2024 amesekiliza kero za wananchi katika ukumbi wa uwekezaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kutoa maamuzi mbalimbali.

Mhe. Mtambi amemsikiliza Bibi Joyce Marwa Matiku (66) ambaye nyumba yake pamoja na shamba viliuzwa mwaka 2017 na mtoto wake wa kwanza Joseph Marwa Matiku (49) na kesi imeenda hadi mahakama kuu lakini haikuwa inapata maamuzi kutokana na makosa ya ufunguaji wa kesi kwa sababu hakuwa na wanasheria wa kumsimamia.

Katika maamuzi yake, Mhe. Mtambi amempatia mawakili watakaomsaidia kufungua upya kesi hiyo na kumueleza Bibi Matiku kuendelea kuishi katika nyumba hiyo iliyouzwa mpaka maamuzi ya Mahakama yatakavyotolewa baada ya kuwa amesimamiwa na mawakili aliompatia yatakapoamuru vinginevyo.

Mhe. Mtambi amewasilikiza wananchi wa Kijiji cha Bumangi, Wilaya ya Butiama ambao eneo lao walilopanga kujenga soko liligawiwa kwa makosa na dalali wa mahakama katika kesi ya talaka baina ya wanandoa wawili na eneo hilo kupewa mke wa wanandoa hao.

 Katika maamuzi yake, Mhe. Mtambi amewataka viongozi hao kuendelea kulitumia eneo lao lililogawiwa katika kesi ya talaka ya wanandoa hao na kama kuna mtu atakuja kuwaondoa wawataarifu viongozi wa Wilaya ya Butiama na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Kanali Mtambi amewasikiliza wananchi wanaoidai fidia Manispaa ya Musoma baada ya maeneo yao kutumika kujenga shule za Sekondari za kata na kuwataka kufika jumatatu tarehe 8 Julai, 2024 wakiwa na vielelezo vyao ambapo pia Mkurugenzi na baadhi ya maafisa kutoka Manispaa ya Musoma wataitwa kujibu hoja zao.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa kibali kwa mwananchi aliyekuwa na shamba katika eneo lililouzwa kwa Wakala wa Vipimo kwenda kukata miti yake iliyokuwa katika eneo hilo kabla halijauzwa kwa Wakala wa Vipimo.

Katika kusikiliza kero za wananchi, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bwana Dominicus Lusasi, Kamati ya kusikiliza Kero za wananchi aliyoiunda na baadhi ya Maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa