• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi apongeza Serengeti kwa kukamilisha bweni

Posted on: September 23rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ametembelea Shule ya Sekondari Ngoreme, Wilaya ya Serengeti kukagua utekelezaji wa maagizo aliyotoa tarehe 13 Agosti, 2024 kuhusu Halmashauri kukamilisha bweni lililojengwa kwa michango ya wananchi na wadau na kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa hatua iliyofikia katika ukamilishaji wa bweni hilo.

Mhe. Mtambi ametoa pongezi hizo baada ya kukuta mafundi wakiwa wanaendelea na shughuli za ukamilishaji ikiwemo kujenga ngazi kwenye milango ya kuingilia na kupaka rangi awamu ya pili kwa ndani ya jengo hilo ambalo lilikuwa limeachwa bila kukamilishwa kwa miaka saba.

“Ninaipongeza sana Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa hatua iliyofikia katika ukamilishaji wa bweni hili na kuitaka kukamilisha ndani ya wiki sita walizopewa na kuwasilisha taarifa kuhusiana na utekelezaji wa agizo hilo” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi ameitaka Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa baada ya wiki sita alizotoa kukamilika, wanafunzi waliokuwa wanalala katika vyumba vya madarasa wanahamia katika bweni hilo baada ya kukamilika.

Aidha, ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kukamilisha uingizaji wa maji na umeme katika bweni hilo ili wanafunzi wakae sehemu salama kwa matumizi yao.

Mhe. Mtambi amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Serengeti kwa usimamizi wake katika utekelezaji wa maagizo hayo na kumtaka kuhakikisha kuwa Halmashauri inakamilisha umaliziaji wa bweni hilo ndani ya muda waliyopewa.

Mhe. Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya, Halmashauri na taasisi za Serikali kutoa ushirikiano kwa viongozi wa kimila na machifu waliopo katika maeneo yao.

Mhe. Mtambi amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Serengeti kuhakikisha wataalamu kutoka SENAPA, TAWA na TFS wanashughulikia tatizo la nyani na gendere katika eneo hilo la Ngoreme kuanzia tarehe 21 Septemba, 2024 ili wananchi waweze kuzalisha chakula katika mashamba yao. 

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ngoreme Mwalimu Daniel Mgaya amesema ujenzi wa bweni hilo umefanywa na Jumuiya ya Maendeleo Ngoreme na kuwekewa jiwe la msingi na Mwenge wa Uhuru mwaka 2017.

Mwalimu Mgaya amesema baada ya Mkuu wa Mkoa kutoa maelekezo ya kukamilisha ujenzi wa bweni hilo tarehe 13 Agosti, 2024, tarehe 14 Agosti, 2024 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Serengeti alileta wataalamu kwa ajili ya kufanya tathmini ya kazi na gharama inayohitajika na baadaye alileta shilingi milioni 26.6 kwa ajili ya ukamilishaji wa bweni hilo.

Mwalimu Mgaya amesema shughuli zilizofanyika mpaka sasa ni pamoja na kufunga dari, sakafu, kukamilisha madirisha, kupaka rangi ndani na nje na kuongeza kuwa shughuli zinazoendelea kwa sasa ni kupaka rangi kwa mara nyingine kwa ndani na kujenga ngazi katika jengo hilo.

Kwa mujibu wa Bwana Mgaya kazi ambazo hazijakamilishwa ni kutengeneza meza ya kunyooshea nguo na kufulia katika bweni hilo pamoja na kuingiza umeme na maji katika bweni hilo.

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mara aliambatana na Wakuu wa Wilaya za Musoma, Tarime na Serengeti, Diwani wa Kata ya Kenyamonte na wananchi wa eneo hilo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa