• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi apongeza mpango wa mikopo kwa wajasiriamali

Posted on: October 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amekutana na kuzungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Bwana Amon Anastaz Mpanju ambaye yupo Mkoani Mara kwa lengo la kuzungumza na wafanyabiashara wadogo wadogo kuhusiana na mikopo mipya kwa wajasiriamali itakayotolewa na Serikali kupitia Benki ya NMB.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi ameipongeza Serikali kwa kuanzisha mikopo kwa ajili ya wajasiriamali na kuongeza kuwa jambo hili limefika wakati muafaka kwa kuwa amekuwa akipokea maombi kutoka kwa wajasiriamali na hususan ambao walikuwa hawapewi mikopo inayotolewa na Halmashauri.

“Ninaipongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita kuja na wazo hili, kuna kundi kubwa la wananchi ambao walikuwa hawawezi kupata mikopo ya Halmashauri lakini na wao sasa watanufaika na mikopo hii itakayotolewa na Serikali” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kwa wananchi kupata uhakika wa mikopo yenye riba nafuu, itawasaidia kuanzisha na kuendeleza biashara zao na kuachana na mikopo inayotolewa na taasisi ambazo hazijasajiriwa ambayo inawaumiza wajasiriamali.

Kwa upande wake, Bwana Mpanju amesema mpango wa Serikali kutoa mikopo upo katika hatua nzuri ambapo tayari Benki ya NMB imeshinda kwa ajili ya kutoa mikopo hiyo kwa riba ya asilimia  saba isiyoongezeka.

Bwana Mpanju amesema ili kunufaika na mikopo hiyo wajasiriamali wanatakiwa kuwa na vitambulisho vya wajasiriamali ili kuweza kutambulika shughuli wanazofanya na kuweza kunufaika na mikopo hiyo ya wajasiriamali.

Bwana Mpanju amesema vitambulisho vya wajasiriamali vinatarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe 17 Oktoba, 2024 katika Mkoa wa Arusha wakati utoaji wa mikopo kwa wajasiriamali unatarajiwa kuzinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Novemba, 2024.

Bwana Mpanju ameeleza kuwa mikopo hii itawasaidia wajasiriamali kukuza mitaji yao kwa sababu haina kikomo cha kukopa kutegemeana na makubaliano yatakayofikiwa kati ya mjasiriamali na Benki ya NMB na wazo la mjasiriamali katika biashara anayotegemea kuifanya.

Bwana Mpanju pia amezungumza na wajasiriamali wa Wilaya ya Musoma katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara ambao amewataka viongozi wa wajasiriamali kuwahamasisha wajasiriamali kupata vitambulisho vya wajasiriamali vitakavyowasaidia kupata mikopo hiyo yenye riba nafuu.

Akiwa kwenye mazungumzo hayo, Bwana Mpanju ametolea ufafanuzi wa hoja mbalimbali zilizotolewa na wajasiriamali walioshiriki kikao hicho na kuwahamasisha kuwahamasisha wenzao kuchukua kadi za wajasiriamali.

Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na maafisa kutoka Manispaa ya Musoma na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa