• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aongoza ujumbe wa Tanzania Maadhimisho ya 13 ya Siku ya Mara

Posted on: September 14th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Afred Mtambi leo ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Maadhimisho ya 13 ya Siku ya Mara yanayofanyika kuanzia tarehe 12 Septemba, 2024 hadi tarehe 16 Septemba, 2024 katika Mji wa Sekenani, Narok nchini Kenya. 

Mhe. Mtambi na ujumbe wake uliwasili katika Mji wa Narok jana jioni na leo Kanali Mtambi pamoja na viongozi wengine wamepanda miti wa kumbukumbu ya Maadhimisho ya 13 ya Siku ya Mara katika Chuo Kikuu cha Maasai Mara Mjini Narok na baadae kushiriki katika Kongamano la kisayansi kuhusu uhifadhi wa ikolojia ya bonde la Mto Mara lililofanyika katika ukumbi wa chuo hicho.  

Katika maadhimisho haya, Mhe. Mtambi ameambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerard Musabila Kusaya, Wakuu wa Wilaya, Meya na Wenyeviti wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na baadhi ya maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri za Mkoa wa Mara. 

Wengine waliopo katika msafara huo ni wawakilishi wa Wizara ya Maji, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, Wizara ya Maliasili na Utalii, maafisa kutoka Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) na Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC).  

Wengine walioshiriki maadhimisho haya ni maafisa kutoka mashirika yanayohusiana na uhifadhi katika Bonde la Mto Mara na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, baadhi ya wafanyabiashara, vikundi vya burudani na Waandishi wa Habari kutoa Mkoa wa Mara. 

Ratiba ya maadhimisho haya iliyotolewa na Serikali ya Kenya inaonyesha kuwa ufunguzi rasmi wa maadhimisho haya ulifanyika tarehe 12 Septemba, 2024 na Gavana wa Jimbo la Narok huku shughuli za maonyesho ya bidhaa mbalimbali za wafanyabiashara na wajasiriamali, michezo na burudani, yanafanyika kuanzia Septemba 12 hadi tarehe 15 Septemba, 2024 ambayo ndio siku ya kilele.  

Katika ufunguzi rasmi wa maonyesho haya, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Dkt. Vincent Naano Anney aliyekuwa aliambatana na wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara.  

Tarehe 13 Septemba, 2024 kulikuwa na shughuli za michezo, upandaji wa miti na shughuli za uhifadhi katika Msitu wa Mau uliopo katika eneo hilo huku maonyesho na michezo yakiendelea katika Mji wa Sekanani.  

Leo tarehe 14 Septemba, 2024 shughuli za michezo na maonyesho zinaendelea katika Mji wa Sekanani huku Kongamano la Kisayansi kuhusu uhifadhi wa Mto Mara limefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo Kikuu cha Maasai Mara, katika Mji wa Narok. 

Kesho tarehe 15 Septemba, 2024 kilele cha maadhimisho haya kinatarajiwa kutafanyika katika Mji wa Sekanani kwa shughuli za maonyesho ya biashara, burudani na mikutano ya hadhara.  

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya 13 ya Siku ya Mara ni Kwa Pamoja:  Tuhifadhi Bonde la Mto Mara kwa Bioanuai Endelevu na Ustahimilivu wa Tabia nchi” yaani “Flowing Forward Together: Conserving the Mara Basin Ecosystem for Sustainable Biodiversity and Climate Resilience.”  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa