• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi amtaka mkandarasi mradi wa maji Rorya/Tarime kufanyakazi usiku na mchana

Posted on: July 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 22 Julai, 2025 ametembelea mradi wa maji wa Tarime/Rorya na kukutana na Mkandarasi, Mkandarasi Mshauri pamoja na msimamizi mkuu wa mradi huo na kumtaka mkandarasi kufanyakazi usiku na mchana kukamilisha mradi huo.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo ambayo ilionyesha kuwa mradi huo umetekelezwa kwa asilimia 14.5 mpaka sasa na kumtaka mkandarasi kukamilisha mradi huo kwa muda uliopangwa.

“Sisi viongozi tutakuwa tunatembelea mradi huu usiku na mchana na eneo lolote unapotekelezwa ili kujiridhisha kuwa kazi zaukamilishaji wa mradi huu zinaendelea wakati wote, na tutachukua hatua kama kuna uzembe wa aina yoyote” amesema Mhe. Mtambi.  

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka wote wanaohusika na usimamizi wa mradi huo kuhakikisha kuwa kasi ya utekelezaji wa mradi huo inaridhisha na kama kuna changamoto kutoa taarifa kwa viongozi mara moja.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA) Mhandisi Nicas Mugisha amesema mradi huo ulianza tarehe 23 Januari, 2023 na unatarajiwa kukamilika Septemba, 2026 kwa gharama ya shilingi bilioni 134.

Mhandisi Mugisha ambaye pia ni msimamizi mkuu wa mradi huo amesema mpaka sasa mkandarasi wa mradi huo amelipwa malipo ya awali na malipo mengine ya awamu mbili na jumla ya shilingi 24,413,789,082 na mkandarasi haidai Serikali lakini utekelezaji wa mradi huo unaenda taratibu sana.

“Mradi huu ni muhimu kwa kuwa ukikamilika utaimarisha upatikanaji wa maji kwa wakazi 729,496 wa vijiji 37 za Wilaya ya Rorya na Tarime” amesema Bwana Mugisha na kuongeza kuwa mpaka sasa mradi umeajiri Watanzania 115 na waajiriwa wanatarajiwa kuongezeka hadi kufikia 819 kwa kadiri mradi unavyoendelea kutekelezwa.

Mhandisi Mugisha amesema shughuli kubwa iliyofanyika ni ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji lita milioni tatu eneo la Mogabiri ambalo limekamilika, ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji lita milioni moja eneo la Sirari na Kituo cha kusukuma maji Gamasara pamoja na chujio la maji katika chanzo cha mradi huo unaendelea.

Kwa upande wao Meneja wa Mradi Adam Zhu kutoka kwa Mkandarasi wa mradi huo China Civil Engineering and Construction Corporation (CCECC) amekiri ucheleweshaji katika utekelezaji wa mradi huo na kuahidi kuwa hadi kufikia Desemba, 2025 kampuni hiyo itakuwa imekamilisha ujenzi wa miundombinu yote mikubwa katika chanzo cha maji Nyamagaro, Rorya na

Bwana Adam Zhu amesema kuwa kuwa mradi huo umechelewa kwa sababu mkandarasi alichelewa kupokea fedha na kuchelewa kwa baadhi ya vifaa vilivyoagizwa ambavyo kwa sasa vimeshafika Bandari ya Dar es Salaam.  

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara ametoa hadi tarehe 30 Agosti, 2025 Halmashauri ya Mji wa Tarime kufanya maboresho madogo madogo katika Shule ya Sekondari ya Tarime na kufuatilia maombi ya mabweni ya nyongeza katika shule hiyo ili kutatua changamoto za wanafunzi.

Mhe. Mtambi ametoa maagizo hayo baada ya kukagua na kuzungumza na baadhi ya wanafunzi wa kidato cha sita katika shule hiyo ambao walimweleza kuhusiana na changamoto zinazowakabili ikiwemo upungufu wa mabweni, matundu ya vyoo, taa madarasani, meza na viti na upungufu wa maji.  

Mhe. Mtambi ameitaka shule hiyo kuanzisha mfumo ambao utawawajibisha wanafunzi watakaobainika kuhusika na upotevu wa taa madarasani kwa kuanzisha mfumo wa kutambua wanaotumia vyumba vya madarasa kila wakati ili vifaa vinapoibiwa wawajibishwe.

Akiwa shuleni hapo Mhe. Mtambi amewataka wanafunzi hao kubadilika na kulinda vifaa vya shule kwa manufaa yao na amemuagiza Mkurugenzi wa Mjia wa Tarime kutoa pilau na nyama kwa wanafunzi hao siku ya Jumamosi na Jumapili za wiki hii.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Tarime Mwalimu Maro Chenge amesema mapungufu hayo kwa kiasi kikubwa yametokana na ongezeko la wanafunzi kutoka uwezo wa awali 780 hadi 932 waliopo sasa katika shule hiyo.

Mwalimu Chenge amesema kwa sasa shule inaupungufu wa viti na madawati 195 na ili kukabiliana na upungufu huo na ili kama jitihada za dharura za kukabiliana na upungufu huo, wanafunzi wamepewa mabenchi ambayo wanakalia kwa sasa.

Aidha, kuhusu taa, Mwalimu Maro amesema shule imekuwa inafunga taa ambazo zinaibiwa mara kwa mara jambo ambalo linasababisha madarasa mengi kukosa mwanga wa kutosha kutokana na kuwa na taa chache.

Mhe. Mtambi ametembelea maeneo hayo ikiwa ni sehemu ya ziara ya Kamati ya Usalama ya Mkoa kutembelea Wilaya za Rorya na Tarime kukagua miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 15-23 Agosti, 2025.

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Tarime, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Rorya, Kamati ya Wataalamu ya Mkoa, Wakuu wa Taasisi za umma, Menejimenti na watumishi wa Halmashauri za Rorya, Mji wa Tarime na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi amtaka mkandarasi mradi wa maji Rorya/Tarime kufanyakazi usiku na mchana

    July 22, 2025
  • RC Mtambi amtaka mkandarasi kukamilisha mradi wa maji Serengeti kwa wakati

    July 21, 2025
  • Mtambi ataka maboresho maandalizi ya UMISETA/UMETASHUMTA

    July 08, 2025
  • Mtambi awapongeza 2,891 kwa kupata daraja la kwanza

    July 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa