• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ampokea Meja Jenerali Gaguti

Posted on: February 18th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 18/2/2025 amempokea na kuzungumza na Mkuu wa Utumishi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Meja Jenerali Marco Gaguti na ujumbe wake waliopo katika ziara ya kikazi katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika mapokezi hayo yaliyofanyika ofisini kwake, Mhe. Mtambi amesema hali ya usalama ya Mkoa wa Mara ni shwari na wananchi wanaendelea kufanya shughuli zao za kawaida za maendeleo.

Mhe. Mtambi amelipongeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kazi nzuri wanayoifanya kulinda amani na usalama wa nchi na hususan katika maeneo ya mipaka ya Tanzania.

Mhe. Mtambi amelishukuru JWTZ kwa ushirikiano wanaoutoa kwa Serikali ya Mkoa na kuahidi kuwa viongozi na Kamati ya Usalama ya Mkoa itaendelea kutoa ushirikiano kwa JWTZ katika utekelezaji wa majukumu yao katika Mkoa wa Mara.  

Kwa upande wake, Meja Jenerali Gaguti akizungumza katika mapokezi hayo amempongeza  Mkuu wa Mkoa wa Mara na Kamati ya Usalama ya Mkoa kwa kuhakikisha hali ya amani na utulivu inakuwepo katika Mkoa wa Mara jambo ambalo amesema linawawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za kujiletea kimaendeleo.

“Kutokana na amani na utulivu uliopo, wananchi wanaendelea kufanya shughuli zao za kujiletea maendeleo bila ya kuwa na hofu ya aina yoyote ile” amesema Meja Jenerali Gaguti.

Meja Jenerali Gaguti amemshukuru Mkuu wa Mkoa na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara kwa ushirikiano wanaoutoa katika jeshi hilo 

Meja Jenerali Gaguti na ujumbe wake wapo katika ziara ya kawaida ya kikazi kwa siku mbili katika Mkoa wa Mara kuanzia leo na akiwa katika ziara hiyo ameambtana na maafisa mbalimbali kutoka makao makuu ya JWTZ.

Mapokezi hayo yamehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya, Mshauri wa Mgambo wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Kikosi cha JKT Rwamkoma, Mkuu wa Kambi ya JWTZ Makoko.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa