• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

Posted on: May 9th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha tathmini ya mbio za mwenge mwaka 2024 na kukabidhi tuzo ya pongezi kwa Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kushika nafasi ya kwanza kimkoa na kinyago kwa Manispaa ya Musoma kwa kushika nafasi ya mwisho kimkoa katika mbio hizo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi kinyago hicho, Mhe. Mtambi ameagiza kinyago hicho kipokelewe na Mkuu wa Wilaya ya Musoma akiambatana na Katibu Tawala, Mkurugenzi wa Manispaa na Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Manispaa ya Musoma.

“Kinyago hiki kikae ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma mpaka atakapopatikana Mkuu wa Wilaya mwingine ambaye Wilaya yake itakuwa imefanya vibaya wa kumpokea” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kinyago kilichotengenezwa sio kibaya sana kama alivyoagiza na kuitaka Manispaa ya Musoma kulipa gharama za kutengeneza kinyago hicho ili kutoa fundisho kwa Halmashauri nyingine za Mkoa wa Mara kufanya vizuri zaidi katika mbio za mwenge kwa miaka inayokuja.

Aidha, Mhe. Mtambi ametoa tuzo ya pongezi kwa Halmashauri ya Mji wa Bunda ambayo imeongoza kimkoa kwa kupata alama 73.12 na kushika nafasi ya 59 kitaifa pamoja na kuwa mradi mmoja ulikataliwa katika mbio hizo lakini vigezo vingine ilifanya vizuri.

Mhe. Mtambi amezitaka Wilaya kuwa makini katika maandalizi ya mbio za mwenge za mwaka 2025 na kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika mbio za mwenge za mwaka 2024 na kuzipongeza Wilaya ambazo tayari zimeanza kufanya maandalizi.

Akiwasilisha tathmini ya mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024, Mratibu wa Mbio za Mwenge Mkoa wa Mara Bwana Fidel Baragaye amesema katika mbio hizo Mkoa ulishika nafasi ya 16 kati ya mikoa 31 iliyopo hapa nchini.

Bwana Baragaye amesema Halmashauri iliyofanya vizuri ni Halmashauri ya Mji wa Bunda iliyopata alama 73.12 na kitaifa ikawa nafasi ya 59 na Halmashauri iliyofanya vibaya ilikuwa ni Manispaa ya Musoma ambayo ilipata asilimia 62.17 na kushika nafasi ya tisa kimkoa na kitaifa ilishika nafasi ya 158.

Bwana Baragaye ameeleza kuwa changamoto zilizokuwepo ni pamoja na kukosekana kwa nyaraka kwenye baadhi ya miradi, nyaraka zenye mapungufu, uwepo wa stakabadhi zenye mashaka, kuwepo kwa taratibu za manunuzi zilizokiukwa na kutokuzingatia kwa ukamilifu kigezo cha uwezeshaji wa vijana iliyokuwa na vipengele vya mradi wa vijana uliotakiwa kutembelewa na Mwenge na maandalizi ya kongamano la vijana.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka ameupongeza Mkoa wa Mara kwa kuanzisha utaratibu huo wa kutoa vinyago kwa wanaofanya vibaya ili kutoa hamasa kwa Wilaya kufanya vizuri zaidi.

Mhe. Chikoka amesema Wilaya ya Musoma imejipanga kuhakikisha kuwa katika miaka inayofuata haitafanya vibaya tena na kuwataka Wakuu wa Wilaya wengine wajiandae kuchukua kinyago hicho.

Kikao cha tathmini ya mbio za mwenge mwaka 2024 na maandalizi ya mbio za mwenge 2025 kimehudhuriwa na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Waratibu wa Mbio za Mwenge wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa