• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi akabidhi magari RUWASA

Posted on: September 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza hafla fupi ya kukabidhi magari mawili yaliyotolewa na Serikali kwa ajili ya Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mara yatakayotumika katika Wilaya za Tarime na Serengeti.

Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo, Mhe. Mtambi amewataka watendaji wa RUWASA waliokabidhiwa magari hayo kuhakikisha kuwa magari hayo yanatumika vizuri na yawawaongezea kasi ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

“Kwa sasa RUWASA Mkoa wa Mara mna jumla ya magari matano ukijumlisha na magari matatu yaliyokuwepo na pikipiki 35, ni matumaini yangu kuwa magari haya yatatumika kuboresha huduma za upatikanaji wa maji kwa wananchi” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, ameitaka Mhe. Mtambi amesema RUWASA imepanga kununua pikipiki 25 ili kuimarisha suala la usafiri kwa wataalamu katika kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Mara.

Kanali Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya kusimamia matumizi ya magari hayo ili yadumu kwa muda mrefu na yatumike kutoa huduma kwa wananchi wa Wilaya hizo.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Mkoa wa Mara Mhandisi Tulimpoki Mwakalukwa ameishukuru Serikali kwa kutoa magari hayo ambayo amesema walikuwa wanayahitaji sana kama kitendea kazi muhimu.

Mhandishi Mwakalukwa amesema tayari Serikali ilileta amagari mengine matatu ambayo yaligawiwa kwa Ofisi ya RUWASA Mkoa wa Mara, Wilaya ya Butiama na Wilaya ya Bunda wakati gari zilizokabidhiwa leo ni kwa ajili ya Wilaya ya Serengeti na Wilaya ya Tarime.

Kwa mujibu wa Mhandisi Mwakalukwa, kwa sasa Wilaya ambazo hazina magari ni Musoma na Rorya ambayo yameshaombwa Serikalini.

Mhandisi Mwakalukwa amemshukuru Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso kwa kuidhinisha manunuzi na kuugawia Mkoa wa Mara magari hayo ambayo ameahidi kuyasimamia kwa ukaribu katika matumizi yake.

Kwa upande wake, Mhandisi wa RUWASA Wilaya ya Tarime Mhandisi Malando Mashapu ameipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa vitendea kazi muhimu kwa RUWASA Wilaya ya Tarime.

Mhandisi Mashepu ameahidi kuwa magari hayo yatawasaidia katika kuwafikia wananchi katika maeneo yao na kuhakikisha wanapata maji na kutatua changamoto za maji kwa wakati.

Hafla ya kukabidhi magari hayo imehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Maafisa wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, RUWASA na Halmashauri za Mkoa wa Mara.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa