• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aitaka Rorya kusimamia makusanyo

Posted on: June 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kusimamia ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha makusanyo yanapelekwa benki mapema ili kupunguza hoja za ukaguzi.

Mhe. Mtambi ameeleza hayo wakati akizungumza katika kikao cha Baraza Maalum la Madiwani la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG)kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya na kumtaka Mkuu wa Wilaya na Baraza kusimamia upelekwaji wa makusanyo benki. .

“Mkurugenzi hakikisha hamna fedha mbichi (fedha iliyokusanywa kabla ya kufikishwa benki)  inayotumika, fedha zote ziende benki mara baada ya makusanyo, zisikae kwenye mikono ya watu” amesema Mhe. Mtambi .

Kanali Mtambi amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kusitisha mabadiliko ya Mhasibu wa Mapato katika Halmashauri hiyo hadi fedha zote ambazo zilikusanywa na kutokuwasilishwa benki ziwe zimerejeshwa.

Mhe. Mtambi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri kuwasilisha kwenye Baraza la Madiwani orodha ya biashara zote zilizofungwa ili wafanye uhakiki wa uhalisia wa madai ya biashara zaidi ya 2,000 kufungwa katika Halmashauri hiyo jambo ambalo lilipingwa na baadhi ya madiwani walioongea.

Aidha, Mhe. Mtambi ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara kufuatilia kesi za wakusanya mapato ambao hawajawasilisha fedha benki na kusababisha hoja ya ukaguzi.

Mhe. Mtambi ameitaka halmashauri hiyo kupanua wigo wa vyanzo vya mapato kulingana na mazingira ya Halmashauri hiyo ikiwa ni pamoja na kuangalia namna ya kuwavutia watalii na wafanyabiashara kuwekeza katika Halmashauri hiyo.

Awali, CAG alihoji makusanyo kutokuwekwa benki kiasi shilingi 102,860,351 hata hivyo menejimenti ilieleza kuwa shilingi 22,382,030 zilikuwa zimerejeshwa na kuwekwa benki;  shilingi 44,180,836 zimeombewa kufanyiwa marekebisho yaliyokuwa yametokana na dosari za mfumo wa mapato (LGRCIS) na kiasi 36,297,485 hakijawekwa benki.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa  wahusika wa shilingi 11,128,450 kesi yao ipo katika uchunguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU) na wahusika wa shilingi 25,169,035 wamepewa muda hadi kufikia Juni 30, 2024 wawe wameweka fedha zote benki.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa