• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aitaka Rorya kulipa deni la Wizara ya Ardhi

Posted on: June 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 24 Juni, 2024 amelitaka Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kusimamia urejeshwaji wa shilingi bilioni moja zilizokopwa kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutekeleza  mradi wa Kupanga, Kupima na Kumirikisha ardhi (KKK) katika Halmashauri hiyo.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo wakati aliposhiriki Baraza Maalum la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) za mwaka 2022/2023 lililofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.  

“Halmashauri iweke mpango makakati wa kurejesha deni hilo ili kujenga mahusiano mazuri na kupata uwezekano wa kukopa tena huko mbeleni ” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi pia amekumbushia agizo lake la kumrejesha Afisa Ardhi aliyehamishiwa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kurejea Rorya kujibu hoja za ukaguzi zilizotokana na utekelezaji wa mradi wa KKK katika Halmashauri hiyo.

Kanali Mtambi amewataka madiwani kuvuta subira wakati Katibu Tawala wa Mkoa akiendelea kumfuatilia mtumishi huyo ambaye aliahidi kurepoti katika Halmashauri hiyo tarehe 24 Juni, 2024 kuja kujibu hoja za ukaguzi.

Mhe. Mtambi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha manunuzi yanafanyika kupitia mfumo wa NEST na Baraza la Madiwani na watendaji wanapata mafunzo ya mfumo na Sheria ya ununuzi wa umma ya mwaka 2023 na kanuni zake ili manunuzi ya umma yafanyike kwa kufuata sheria.

Mhe. Mtambi amelitaka Baraza la Madiwani kusimamia lipaji mikopo ya madiwani katika benki za NMB na CRDB ambazo zilikatwa katika malipo ya kawaida ya madiwani lakini hayakupelekwa katika benki hizo kulipa mikopo hiyo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Kusaya ameeleza kuwa mhusika alipewa maagizo ya kurejea Rorya kwa ajili ya kujibu hoja hata hivyo hakurejea na badala yake alileta barua yenye maelezo kuwa alikuwa anaumwa na kutoa maelezo mbalimbali kuhusu hoja za ukaguzi kuhusu mradi huo.

Bwana Kusaya ameeleza kuwa mara ya mwisho alipoongea nae aliahidi kurepoti Halmashauri ya Wilaya ya Rorya tarehe 24 Juni, 2024 kwa ajili ya kusaidia kujibu hoja za ukaguzi kuhusu mradi huo na kuahidi kuwa asipowasili siku hiyo Mkoa ungemchukulia hatua za kiutumishi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mheshimiwa Gerald Ng’onga ameomba Afisa Ardhi huyo arejeshwe Rorya ili aisaidie Halmashauri hiyo kujibu hoja za mradi wa kupanga, kupima na kumirikisha ardhi (KKK) uliotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Ng’ong’a amesema kutokana na mradi huo Halmashauri ilipata hoja za ukaguzi 21 kutokana na mradi wa KKK na kati ya hoja hizo 14 zimejibiwa na kufungwa lakini bado hoja saba hazijafungwa.

Kwa upande wao madiwani wa Halmashauri hiyo waliopata nafasi ya kuzungumza walielezea kusikitishwa kwao na kitendo cha Afisa Ardhi huyo kuchelewa kuwasili na kuendelea kukamishwa majibu ya hoja za mradi huo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa