• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aitaka Butiama kuboresha ufaulu

Posted on: May 31st, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo amefanya kikao na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na kuwawataka Wakuu wa Shule za Sekondari na Walimu Wakuu wa Shule za msingi kuboresha ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya kitaifa ya darasa la saba na kidato cha nne.  

“Kidato cha Sita mnafanya vizuri lakini shule ya msingi na kidato cha nne bado kunajitihada zinahitajika kuboresha elimu ya watoto wetu” amesema Mhe. Mtambi na kuwataka Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule kuchukua hatua kurekebisha hali hiyo.

Mhe. Mtambi amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Butiama kuwafuatilia Afisa Elimu Sekondari na Afisa Elimu wa Shule za Msingi ili wazisimamie shule zilizopo katika Halmashauri hiyo ili ziweze kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa.   

Mhe. Mtambi amemtaka Mkuu wa Wilaya kuitisha kikao cha wazazi wote katika shule za umma ambazo hazina mwitikio wa kuchangia chakula shuleni na fedha za taaluma kwa ajili ya kuwalipa walimu wa kujitolea na kuwahamasisha kuchangia michango hiyo ili shule hizo ziweze kufanya vizuri.

Kanali Mtambi amesema ofisi yake itaanza kutoa tuzo ya vinyago kwa shule ambazo zinafanya vizuri na ambazo hazifanyi vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa ili kutoa motisha kwa shule hizo kufanya vizuri katika mitihani inayofuata.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amewataka walimu kukemea vitendo vichafu vinavyofanywa kwa wanafunzi mashuleni na kuwataka walimu kuwalinda, kuwaelimisha na kufuatilia tabia za wanafunzi wao na kama kuna mabadiliko toeni taarifa mapema.

Mhe. Mtambi amesema kuna taarifa za uwepo wa vitendo vya ushoga, ubakaji na ulawiti katika baadhi ya shule na katika jamii zikiwahusisha watoto wanaosoma jambo ambalo amesema halikubaliki, na kuwataka walimu wafuatilie wanafunzi wao.

Kwa upande wake, Mwalimu mkuu wa Sekondari wa Shule ya Sekondari ya Butiama Bibi Grace Isomba amesema kuwa mwaka 2021 shule yake ilipata ufaulu wa asilimia 87, mwaka 2022 asilimia 87 na mwaka 2023 walipata asilimia 84 .  

Bibi Isomba ameeleza kwa mwaka 2023 ufaulu ulishuka kutokana na ongezeko la idadi ya wanafunzi katika shule hiyo na kupungua kwa idadi ya walimu na baadhi ya wanafunzi kutoka maeneo ya mbali na shule hiyo mambo ambayo yaliathiri taaluma katika shule hiyo.

Bibi Isomba amesema kuwa changamoto nyingine katika shule hiyo ni asilimia kubwa ya wanafunzi kutopata chakula cha mchana shuleni kwa sababu wazazi wao hawajachangia chakula jambo ambalo linaathiri ujifunzaji na ufundishaji kwa wanafunzi hao.

Bibi Isomba amesema kuwa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 1,242 hata hivyo wanafunzi wanaopata chakula cha mchana shuleni ni takriban wanafunzi 400 tu kwa shule nzima na wanafunzi waliobakia hawapati chakula na hivyo kushinda na njaa.

Akiwa katika Wilaya hiyo, Mkuu wa Mkoa alikagua mradi wa maji Kirumi, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Butiama, barabara za Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika Kata ya Butiama, alifanya kikao na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na kuhitimisha na mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Butiama.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa ameambata na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Butiama, Kamati ya Usalama Wilaya ya Butiama, Mwenyekiti na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama baadhi ya maofisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na watumishi wa Halmashauri ya Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa