• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aitaka Bodi ya Kwangwa kusimamia uboreshaji wa huduma

Posted on: December 12th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 12 Desemba, 2024 amezindua Bodi ya Ushauri ya Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) na kuitaka Bodi hiyo kusimamia uboreshaji wa maboresho katika utoaji wa huduma kwa wananchi.   

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Mhe. Mtambi amesema kuna nafasi ya kuweza kuziboresha huduma hizo baada ya uwekezaji mkubwa katika miundombinu, watumishi na vifaa tiba uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika hospitali hiyo.

“Bodi kama haitavaa viatu vyake, menejimenti ya Hospitali haitafanya kazi vizuri na wananchi hawatapata huduma zinazotegemewa na kupingana na adhma ya Serikali ya awamu ya sita ya kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi ameitaka Bodi hiyo kusimamia Sera, Sheria na miongozo ya Wizara ya Afya kuhusu utoaji wa huduma bure kwa wazee wasiojiweza, wajawazito na watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kupata huduma bure na kupunguza ukiritimba katika utoaji wa misamaha hiyo.

Mhe. Mtambi ameitaka bodi hiyo kutumia uzoefu wao, na taaluma zao katika kuisaidia na kuishauri Hospitali hiyokuwa wabunifu ili iweze kujiendesha na kuboresha huduma kwa wananchi na kupunguza rufaa kwenda katika hospitali nyingine za Rufaa.

Mhe. Mtambi ameitaka Menejimenti ya Hospitali hiyo kujipanga na kupunguza malalamiko ya wananchi kuhusiana na huduma katika Hospitali hiyo na kumwagiza Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kuhakikisha kuwa huduma za vipimo inapatikana katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya muda wote bila kujali usiku, mwisho wa wiki na siku za sikuukuu.

Mhe. Mtambi amesema ofisi yake imejipanga kufuatilia utoaji wa huduma katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki wakati wote kama inavyotarajiwa.

Mhe. Mtambi ametumia nafasi hiyo kuwataka watendaji wa Serikali wa Mkoa wa Mara kuhakikisha kuwa fedha zinazoletwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo inatumika vizuri

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Wizara ya Afya Bi. Glory Laizer amesema Bodi ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere yenye wajumbe kumi imeteuliwa na Waziri wa Afya kwa mujibu wa Sheria tangu Januari, 2024 na itafanyakazi kwa miaka mitatu hadi 2027.

Bi. Laizer amesema mchakato wa uteuzi wa wajumbe wa Bodi hiyo ulianzia Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Mara ambaye mapendekezo ya wajumbe wa bodi hiyo ambayo ina mchanganyiko wa utaalamu na wanaotokana na wananchi wa Mkoa wa Mara na baadaye Waziri wa Afya aliwateua.

Bi. Laize amesema kwa sasa mafunzo ya wajumbe hao pamoja na menejimenti ya Hospitali hiyo yameanza jana ili kuwapitisha kuhusu majukumu na wajibu wa bodi na menejimenti katika utekelezaji wa mipango na uendeshaji wa Hospitali hiyo. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Hospitali hiyo Dkt. Hosea Bisanda amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa watafanyakazi yao kwa ufanisi na watahakikisha katika muda wao wa uongozi wa miaka mitatu wataacha alama channya katika taasisi hiyo.

Dkt. Bisanda amesema kama Bodi hospitali hiyo itoe huduma nzuri na kupunguza rufaa za kwenda Hospitali za Rufaa za Kanda na Hospitali za Taifa kulingana na wataalamu waliopo katika Hopsitali hiyo na kuifanya hospitali hiyo kuwa kimbilio la wananchi wanyonge.

 Hafla ya uzinduzi wa bodi hiyo zimehudhuliwa wajumbe wa Bodi hiyo, wawakilishi kutoka Wizara ya Afya, maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Menejimenti na baadhi ya watumishi wa hospitali hiyo.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa