• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Rorya

Posted on: June 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 24 Juni, 2024 ameshiriki katika Baraza Maalum la Madiwani la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na kuipongeza  Halmashauri hiyo kwa kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo na makusanyo ya Halmashauri.

“Huu ni ushahidi tosha kuwa kuna mshikamano wa dhati katika kuimarisha mifumo ya mapato na matumizi na kusimamia utendaji wa Serikali kwa ujumla” amesema Mheshimiwa Mtambi na kulipongeza Baraza la Madwani kwa usimamizi mzuri wa Halmashauri.

Mhe. Mtambi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kwa ukusanyaji wa mapato ambapo hadi kufikia tarehe 30 Mei, 2024 Halmashauri hiyo ilifanikiwa kukusanya asilimia 97 ya fedha zote zilizopangwa kukusanywa katika mwaka wa fedha 2023/2024.

“Ni matumaini yangu kuwa katika muda uliobakia Halmashauri itakusanya kwa asilimia 100 na zaidi katika mapato yake ya ndani ili yasaidie katika kuboresha huduma za wananchi wa Wilaya ya Rorya” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameliagiza Baraza la Madiwani kuhakikisha Halmashauri inaandaa mpango kazi wa kujibu hoja zote za CAG na maagizo ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Seriklai za Mitaa (LAAC) yaliyotolewa mwaka 2023 na kuchukua hatua kwa wote wanaosababisha hoja za ukaguzi.

Aidha, Mhe. Mtambi ameitaka Halmashauri ihakikishe watumishi na MAdiwani wanapata mafunzo kuhusu Mfumo wa Taifa wa Manunuzi (NEST)  na sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2023 na kanuni zake ili manunuzi ya umma yafanyike kwa kufuata sheria.

Amelitaka Baraza la Madiwani kusimamia utoaji wa mikopo ya vikundi na urejeshaji wa mikopo kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika na mikopo ya Serikali kwa mujibu wa taratibu.

Kanali Mtambi amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa kuratibu mafunzo ya mifumo ya kielektroniki ya Serikali kwa Wakaguzi wa Ndani wa Mkoa wa Mara ili kupata uelewa na kuwawezesha kukagua mifumo hiyo kulingana na taratibu zinazotakiwa.

Mhe. Mtambi ameitaka Menejimenti ya Halmashauri hiyo kuandaa mpango mkakati wa kurejesha fedha zote zilizokopwa kwenye akaunti ya amana  

Kanali Mtambi amelitaka Baraza la madiwani kusimamia ulipaji mkopo wa madiwani katika benki za NMB na CRDB, mkopo wa shilingi bilioni moja uliochukuliwa kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kuhakikisha watumishi wote waliosababisha hoja za ukaguzi wanachukuliwa hatua za kiutumishi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mhe. Gerald Ng’ong’a amesema tangu madiwani hao walipoingia madarakani Halmashauri hiyo imeimarisha ukusanyaji wa mapato na kudhibiti matumizi ya fedha za umma kwa sasa inafanya vizuri.  

Katika ukaguzi huo, Halmashauri ilipata hoja 92 na maagizo ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) matano na hadi kufikia  tarehe 24 Juni, 2024 hoja 38 zilikuwa zimejibiwa na kufungwa, hoja 54 utekelezaji wake unaendelea.

Mhe. Ng’ong’a ameahidi kuwa Halmashauri yake itatekeleza maagizo yote yaliyotolewa katika kikao hicho kwa wakati na kuahidi kuwa Baraza la Madiwani na wataalamu kuendelea kushirikiana katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Wilaya ya Rorya.

Mhe. Ng’ong’a ameeleza kuwa kwa sasa Halmashauri hiyo imeweka mkakati wa kupunguza madeni ya zamani kwa kujitahidi kukusanya mapato ya ndani ya kutosha ili kuyatumia kulipa madeni yake kila wakati.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Rorya, wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Menejimenti na baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa