• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aipongeza Bunda TC kwa usimamizi wa miradi

Posted on: June 28th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 27 Juni, 2024 amefanya ziara katika Halmashauri ya Mji wa Bunda na kuipongeza Halmashauri hiyo kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.  

“Ninawapongeza sana kwa usimamizi wa miradi na ubora wa majengo mnayojenga, hapa kazi inaonekana, mmepata mafundi wazuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, ameitaka Halmashauri hiyo kutunza taarifa za mafundi wake wanaofanya kazi vizuri ili mafundi hao waweze kutumika katika kutekeleza miradi mingine itakayokuja katika Halmashauri hiyo.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ametembelea na kukagua mzani wa ukaguzi wa magari wa Robana uliopo katika Halmashauri ya Mji wa Bunda na kujionea namna mzani huo unaopima magari yakiwa kwenye mwendo unavyofanya kazi.

Akiwa katika mradi huo, Mkuu wa Mkoa ametaarifiwa kuwa mradi umefikia asilimia 95 ya utekelezaji wake na kwa sasa mzani huo umeanza kufanyakazi na kupunguza msongamano wa magari katika mzani wa awali uliokuwepo katika eneo hilo.

Baada ya hapo, Mhe. Mtambi ametembelea Shule ya Sekondari ya Migungani inayoendelea kujengwa katika eneo hilo na kukagua mradi wa vyumba sita vya madarasa na matundu nane ya vyoo unaoendelea kutekelezwa katika eneo hilo.

Akiwa katika shule hiyo, Mkuu wa Mkoa mbali na kukagua ujenzi, amesalimiana na wanafunzi wa kidato cha pili na kidato cha nne wanaoendelea kujisomea katika shule hiyo na kuzungumza na baadhi ya walimu wa shule hiyo waliokuwepo katika eneo la shule.

Baada ya hapo, Mhe. Mtambi ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bunda na kupongeza kuanza kwa utoaji wa huduma katika Hospitali hiyo na kuitaka Halmashauri hiyo kutumia mapato ya ndani kukamilisha majengo ambayo hayajakamilika katika hospitali hiyo.

Mkuu wa Mkoa pia alifanya mkutano na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda na kuwakumbusha watumishi kuhusu uadilifu na kuwataka kurudi kwenye misingi ya utumishi wa umma katika kuwatumikia wananchi.

Mkuu wa Mkoa amehitimisha ziara yake kwa kushiriki kikao cha Baraza la Madiwani la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe. Dkt. Vincent Anney Naano amewapongeza wasimamizi wa ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo.

Mhe. Dkt. Naano amesema mradi huo utakapokamilika utaiwezesha Serikali kutoa huduma za Hospitali ya Mji kwenye hospitali yake badala ya kuendelea kuitumia Hospitali Teule ya Halmashauri ya Mji wa Bunda (DDH) inayomilikiwa na taasisi za kidini iliyopo katika Mji wa Bunda.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambatana na Katibu Tawala wa Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Bunda, wakuu wa taasisi za umma, maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na wasimamizi wa miradi iliyotembelewa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa