• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aipongeza Bunda DC kwa kupata hati safi na makusanyo ya mapato

Posted on: June 28th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara leo tarehe 26 Juni, 2024 ameshiriki kikao cha Baraza la Madiwani cha Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na kuipongeza halmashauri hiyo kwa kupata hati safi ya ukaguzi na ukusanyaji wa mapato.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Mtambi amesema Halmashauri hiyo imepata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo jambo ambalo linaonyesha kuwa kuna kazi kubwa inafanyika katika halmashauri hiyo na ushirikiano kati ya viongozi na watendaji.

“Ninaipongeza Halmashuri kwa kufanikiwa kukusanya shilingi 1,765,822,401 hadi kufikia tarehe 3o Mei, 2024 ambayo ni sawa na asilimia 90.2 ya makusanyo ya shilingi 1,955,676 yaliyopangwa kukusanywa kwa mwaka wa fedha 2022/2023” amesema  Mhe. Mtambi.

Aidha, Mhe. Mtaambi amesema amepata taarifa kuwa hadi kufikia tarehe 25 Juni, 2024 Halmashauri hiyo imefikia asilimia 96 ya ukusanyaji wa mapato ya ndani.  

Mhe. Mtambi ametoa siku saba kwa Halmashauri za Mji wa Bunda na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuwa zimekamilisha mchakato wa kugawana mali na madeni yaliyotokana na iliyokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kabla ya kuanzishwa kwa Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Mhe. Mtambi ameitaka RUWASA kuhakikisha Mji wa Kibara unapata maji safi na salama ya uhakika kwa kuandaa mradi mkubwa wa kusambaza maji katika eneo hilo na kumtaka Mkuu wa Wilaya ya Bunda kufuatilia kwa karibu.

Kanali Mtambi amewataka Madiwani kwa kushirikiana na Watendaji wa Kata na Watendaji wa Vijiji kuhamasisha chakula cha watoto mashuleni na kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ya utawala.

Katika taarifa ya ukaguzi wa CAG, Halmashauri ilipata hoja 78 maagizo ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za (LAAC) 15 kwa kipindi cha kuanzia 2012/2013 hadi 2022/2023, hoja 17 kwenye mfuko wa pamoja wa afya, hoja 9 za mfuko wa vijana na watu wenye ulemavu .

Taarifa hiyo imeonyesha kuwa hoja za nyuma zilikuwa 54 na kati ya hizo hoja mbili zimefungwa,hoja tisa zinaendelea na utekelezaji haujaanza. Imepata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Charles Manumbu amesema Halmashauri ilianza mwaka 2016, madiwani waliopo kwa sasa wameanza 2020 na kwa wakati huo kulikuwa na malalamiko mengi sana.

“Tulisimama kwenye Sheria, kanuni na taratibu na kuchukua hatua mbalimbali za kurekebisha hali hiyo ikiwa ni pamoja na kuwaondoa baadhi ya watumishi waliokuwa hawana mwenendo mzuri na kwa sasa Halmashauri yetu imetulia” amesema Mhe. Manumbu.

Mhe.Manumbu amesema kwa sasa Halmashauri ina miradi mingi ambayo haikamiliki nakutokana na  jiografia ya Halmashauri kukaa vibaya, gharama kubwa inatumika kwenye usafiri kwa watendaji kwenda kusimamia miradi, kukagua na kutoa huduma kwa wananchi.  

“Katika ukusanyaji wa mapato tangu Halmashauri ilipoanza haikuwahi kukusanya mapato kufikia asilimia 90 lakini mwaka huu hadi kufikia sasa tayari Halmashauri imefikia asilimia 96 ya ukusanyaji wa mapato yaliyopangwa kukusanywa mwaka  2023/2024.

Mhe. Manumbu amesema anategemea kuwa mwaka huu Halmashauri hiyo inaweza kufikia asilimia 100 au zaidi ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mara ya kwanza katika historia.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa