• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ahimiza ushirikiano kulinda ikolojia ya Mto Mara

Posted on: September 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi leo ameongoza ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kilele cha Maadhimisho ya 13 ya Siku ya Mara yaliyofanyika katika Mji wa Sekanani, Narok, Nchini Kenya na kuwataka wadau kushirikiana kulinda ikolojia ya bonde la Mto Mara.

 “Kutokana na umuhimu wa bonde la Mto Mara kwa wananchi, wanyama na  shughuli za utalii katika hifadhi zetu za Maasai Mara na Serengeti ni muhimu wadau wote kushirikiana na kulilinda bonde hilo kwa nguvu zetu zote” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema tafiti mbalimbali zimefanyika katika bonde la Mto Mara na kuwataka wataalamu kuhakikisha kuwa tafiti hizo zinatumika kuboresha utunzaji wa mazingira katika bonde la Mto Mara kwa manufaa mapana ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni wa wananchi wanaoishi katika eneo hilo.

Mhe. Mtambi ambaye amemwakilisha Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso, amesema Sera ya Taifa ya Maji ya Tanzania ya mwaka 2022 na Sheria ya Menejimenti ya Rasilimali za Maji zinawahimiza wananchi, taasisi na wadau wote kutunza vyanzo vya maji kwa ajili ya maendeleo endelevu.

Mhe. Mtambi ameipongeza Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) na kamati ya maandalizi kwa kufanikisha maandalizi ya maadhimisho hayo na kuwakaribisha wadau wote katika maadhimisho ya 14 ya Siku ya Mara ambayo yanatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 12 Septemba, 2025 katika eneo litakalopangwa.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) Dkt. Masinde Bwire amesema uhifadhi wa bonde la Mto Mara ni muhimu sana kwa kuwa ni maliasili ya ulimwengu mzima na tunawajibika kuitunza kwa maendeleo maendeleo ya wananchi, wanyama na uhifadhi wa ikolojia kwa maendeleo endelevu.

Dkt. Bwire amezitaka Serikali za Tanzania na Kenya kutenga fedha katika bajeti zake kwa ajili ya shughuli za uhifadhi na upandaji wa miti katika bonde la Mto Mara ili kuilinda ikolojia ya eneo hilo kwa ajili ya kizazi cha sasa na vijavyo.

 Dkt. Bwire amewataka wananchi kuendelea kutunza mazingira ya bonde la Mto Mara na kuwasikiliza wataalamu na watafiti wanavyoshauri kuhusu namna bora ya kuendelea kuhifadhi mazingira ili kuendelea kupata manufaa ya uhifadhi na ikolojia katika bonde hilo.

Ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wafadhili wa Maadhimisho ya 13 ya Siku ya Mara ambao wamewezesha shughuli mbalimbali za maadhimisho hayo kuanzia tarehe 12 Septemba, 2024 hadi leo siku ya kilele cha maadhimisho hayo.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kenya Bwana Abdi Dubat amesema Bonde la Mto Mara liko katika hatari ya kuharibiwa ikolojia yake kutokana na ukataji wa miti, shughuli za kibinadamu na mabadiliko ya tabia nchi.

Bwana Dubat ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amesema ili kukabiliana na hali hiyo, Serikali ya Kenya ina mpango wa kupanda miti bilioni 15 katika kipindi cha miaka kumi katika nchi hiyo na Bonde la Mto Mara limepewa kipaumbele kwa ajili ya kupanda miti huo kutokana na umuhimu wake.

Bwana Dubat amewapongeza wananchi wa Narok pamoja na viongozi kwa shughuli za utunzaji wa mazingira wanazozifanya na kuwataka waendelee kwani ni muhimu wa wanyama, vyanzo vya maji na shughuli za utalii endelevu katika eneo hilo.

Bwana Dubat amewataka wageni wote kutembelea vivutio vya utalii mbalimbali vilivopo Narok na hususan Hifadhi ya Maasai Mara iliyopo katika eneo hilo.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya 13 ya Siku ya Mara ni Kwa Pamoja:  Tuhifadhi Bonde la Mto Mara kwa Bioanuai Endelevu na Ustahimilivu wa Tabia nchi” yaani “Flowing Forward Together: Conserving the Mara Basin Ecosystem for Sustainable Biodiversity and Climate Resilience.” 

Maadhimisho haya yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Tanzania ikiwemo maafisa kutoka    Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Maji na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa  Afrika Mashariki, viongozi na baadhi ya maafisa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri za Mkoa wa Mara.

Wengine waliohudhuria ni wafanyabiashara, taasisi zinazohusika na uhifadhi, wadau, Waandishi wa Habari na vikundi vya utamaduni kutoka Mkoa wa Mara.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa