• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi afanya ziara Musoma DC

Posted on: September 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 18 Septemba, 2024 amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kuzungumza na wananchi, kutembelea migodi ya Polly Gold na Seka iliyopo katika Halmashauri hiyo.

Mhe. Mtambi amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Kigera Etuma na kutoa saa 48 kwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma kutoa taarifa za mahali alipo mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kigera anayedaiwa kutoroshwa na mwanaume wa kijijini hapo huku aliyemtorosha akipata dhamana.

Mhe. Mtambi ametoa maagizo hayo baada ya Mama mzazi wa mwanafunzi huyo kudai kuwa mtuhumiwa ambaye mara ya mwisho alikuwa na mtoto wake ameachiwa na yupo kijijini hapo wakati yeye hajui mtoto wake alipo.

Kanali Mtambi amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Musoma kufuatilia wazazi na walezi wa wanafunzi watano waliopewa mimba katika Shule ya Sekondari Kigera na ambao watuhumiwa hawajakamatwa au walikamatwa na kuachiwa na baadaye kutoroka.

Aidha, Mhe. Mtambi amewahamasisha wananchi wa Kijiji hicho kuacha kufanya starehe kwa kuweka mziki mara kwa mara na kuacha kuzingatia usalama awa watoto wao baada ya baadhi ya wananchi kulalamikia Maafisa Utamaduni kutoa vibali vya muziki mara kwa mara kwa ajili ya watu kupiga muziki katika eneo hilo.

Mhe. Mtambi pia amewataka viongozi na wananchi wa eneo hilo kuhakikisha kuwa miradi ya kuihudumia jamii (CSR) inayotolewa na wamiliki wa migodi ya dhahabu katika eneo hilo inakuwa miradi endelevu itakayochechemua maeneo ya kijiji hicho.

Mhe. Mtambi amesema hamna maana kama wawekezaji hao watapatiwa miradi midogo midogo ambayo inaweza kufanyika kwa michango ya wananchi na ambayo haina tija kwa maendeleo endelevu ya kijiji hicho na wananchi wake, badala yake wawekezaji hao wapewe miradi ya kimkakati itakayokuza uchumi wao.

 Mhe. Mtambi amewaagiza wawekezaji katika migodi ya madini katika eneo hilo kupunguza vumbi barabarani kwa kumwagia maji wakati wanaposafirisha mawe yenye dhahabu ili kulinda afya za wananchi wa kijiji hicho na miundombinu ya barabara.

Akiwa katika mkutano huo, Mhe. Mtambi amewahamasisha wazazi kuchangia chakula cha watoto shuleni baada ya wananchi kushuhudia wanafunzi ambao hawana chakula wakiwa wanawaangalia wanafunzi wengine ambao walikuwa wanakula wakati wa mapumziko ya mchana katika Shule ya Msingi Kigera.

Baada ya mkutano huo, Mhe.Mtambi ameitebelea migodi ya Polly Gold na Seka na kujionea namna uzalishaji unavyofanyika na kujadiliana na migodi hiyo kuhusiana na namna bora ya kupunguza vumbi katika vijiji vinavyopitiwa na magari ya migodi hiyo.

Aidha, ameitaka migodi hiyo kutoa ajira kwa wananchi wanaoizunguka migodi hiyo ili kujenga uhusiano endelevu na wananchi hao.

 Mkuu wa Mkoa katika ziara hiyo aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma, baadhi ya watumishi kutoka Sekretarieti ya Mkoa, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na viongozi wa migodi hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa