• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi afanya ziara Bunda

Posted on: June 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 26 Juni, 2024 amefanya ziara kwa mara ya kwanza katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambapo akiwa katika Halmashauri hiyo amekagua miradi ya maendeleo, kuzungumza na watumishi na kushiriki kikao cha Baraza cha kujibu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Mhe. Mtambi ameanza ziara yake kwa kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Mara inayojengwa katika Halmashauri hiyo na kumwagiza Mkuu wa Wilaya kuhamia kwa muda katika shule hiyo inayotarajiwa kuanza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano kuanzia tarehe 30 Juni, 2024.

“Ninataka uhamie hapa ili kusimamia usafi wa mazingira, marekebisho ya baadhi ya maeneo niliyoagiza na ukamilishaji wa utengenezaji wa samani kwa ajili ya wanafunzi” amesema Mhe. Mtambi na kuitaka Halmashauri hiyo kuyafanyia kazi maagizo yake aliyoyatoa.  

Baada ya hapo, Mhe. Mtambi ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri na nyumba ya wakuu wa idara zinazoendelea kujengwa katika eneo la Mumagunga, Kibara na kuagiza Halmashauri kukamilisha mradi huo haraka ili Mkurugenzi aweze kuhamia.    

Akiwa kwenye mradi huo, Mkuu wa Mkoa amepongeza ubora wa ujenzi wa mradi huo ambao umefikia asilimia 95 ya utekelezaji  na kutoa muda wa miezi miwili Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo awe amehamia na kuleta taarifa ofisini kwake za utekelezaji wa agizo hilo.    

Aidha, Mkuu wa Mkoa pia amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na kumtaka mkandarasi wa mradi huo Suma JKT kukamilisha mradi huo kwa haraka.

Kanali Mtambi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kusafisha mazingira kuzunguka mradi huo na kuandaa upatikanaji wa mahitaji ya ujenzi ili kumrahisishia mkandarasi wa mradi huo kutekeleza mradi  kwa wakati.

Akiwa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda pia Mhe. Mtambi amezungumza na wafanyakazi wa Halmashauri hiyo na kuwakumbusha kufanyakazi kwa bidii na weredi na kuongeza ubunifu ili kuwatumikia kwa ufanisi wananchi.

Mkuu wa Mkoa amehitimisha ziara yake kwa kuhudhuria kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili hoja za CAG  vikao vilivyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Bunda, Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa