• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aagiza RUWASA kurejesha maji bure Nyamikoma B

Posted on: June 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameshiriki kikao maalum cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na kuiagiza Mamlaka ya Maji Vijijini (RUWASA) kupeleka maji bure Shule ya Msingi Nyamikoma B iliyopo katika eneo la Pida, Wilaya ya Butiama.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya wananchi kuwasilisha malalamiko kuhusu RUWASA kukitumia kisima cha shule hiyo kilichochimbwa kwa ufadhili wa Shirika la PCI shuleni hapo na kuyasambaza katika eneo hilo na kuidai shule hiyo kulipa bili za maji kama watu na taasisi zilizopo katika eneo hilo.

“Naagiza maji kwenye shule hii yaletwe haraka na watatumia bure kwa sababu kisima hiki ni cha kwao kilichimbwa na mfadhili wao ili watoto waweze kupata maji kiurahisi, hamna kuwaletea bili za maji” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameagiza kuwa kwa kuwa shule hiyo imetoa kisima chake bure na kuruhusu maji yake yasambazwe kwa wananchi wa maoneo hayo, RUWASA itumie busara kurudisha huduma za maji katika shule hiyo haraka iwezekanavyo.

Mhe. Mtambi amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Butiama kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo na kufuatilia pampu zilizokuwa zimefungwa katika kisima hicho ambazo RUWASA wanadai waliikabidhi kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo na Mwalimu Mkuu anadai ipo RUWASA.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama Bibi Eunice Makere ameeleza kuwa alipokea malalamiko hayo kutoka katika shule hiyo na kufanya kikao na RUWASA, uongozi wa Kijiji na uongozi wa watumia maji na kubaliana maji hayo yarejeshwe kabla shule hazijafunguliwa.

Bibi Makere amesema hata hivyo baada ya maji hayo kuunganishwa katika tanki lililojengwa na RUWASA na shule kutakiwa kulipia maji wanayoyatumia, shule hiyo haijaweza kulipia maji hayo na wanafunzi wa shule hiyo wamekosa maji kutokana na maamuzi hayo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Butiama Mhe. Christopher Marwa Siagi amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa michango yake aliyoitoa katika Baraza hilo maalum inayolenga kuleta tija.

Mhe. Siagi amemuomba Mkuu wa Mkoa kusaidia Shule ya Sekondari ya Mkono iliyopo katika Wilaya ya Butiama kupata maji kutokana na shule hiyo kuwa na wanafunzi wengi na kukosa maji ya uhakika ya kutumia.

Aidha, Mhe. Siagi ameitaka Halmashauri hiyo kutoa taarifa za fedha za miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo pindi fedha zinapoingia ili kukiwezesha Chama cha Mapinduzi kufanya ukaguzi wa miradi inayotekelezwa kutokana na fedha hizo.

Kikao cha Baraza la Madiwani kilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Butiama, Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Hamashauri ya Wilaya ya Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa