• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Msovela Awataka Wakandarasi kukamilisha miradi kwa wakati

Posted on: July 30th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela amewataka wakandarasi waliopata zabuni za kutekeleza miradi ya Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) katika Mkoa wa Mara kukamilisha ujenzi wa barabara hizo kwa wakati.

Bwana Msovela ametoa maagizo hayo leo tarehe 30 Julai 2021 katika hafla ya kusaini mikataba na wakandarasi 122 waliopewa zabuni za kutengeneza barabara, vivuko na madaraja katika wilaya zote za Mkoa wa Mara.

“Niwaombe wakandarasi tujitahidi kukamilisha barabara hizi kwa wakati ili wananchi waweze kupata urahisi wa kusafiri na kusafirisha mizigo yao ikiwemo mazao yao kwa wakati” alisema Bwana Msovela.

Aidha amewataka wakandarasi kulipa tozo zozote za kisheria kwa halmashauri na mamlaka nyingine za serikali kwa wakati ili waweze kuendelea kufanya kazi zao vizuri bila kusmbuliwa.

Katibu Tawala pia amewakumbusha wakandarasi kutekeleza matakwa ya sheria za mazingira wakati wa ujenzi wa barabara hizo ili kuleta maendeleo endelevu ya Mkoa wa Mara.

Bwana Msovela amewaagiza wakandarasi hao kuajiri vibarua katika kazi za ujenzi kwenye miradi huo kutoka maeneo wanayojenga barabara hizo ili wananchi waweze kupata ajira na serikali ipate walinzi wa barabara zake.

Ameitaka TARURA kuimarisha usimamizi na kuhakikisha kuwa barabara hizo zinakamilika kwa wakati, kwa viwango vilivyokubalika na ubora unaoridhisha kwa mujibu wa mikataba.

“Mkisimamia kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni barabara hizi zitakamilika kwa ubora na katika muda uliopangwa kwa mujibu wa mkataba” alisema Bwana Msovela.   

Bwana Msovela ameziomba taasisi za fedha kuongeza ushirikiano wa kibiashara na wakandarasi hao ili barabara za Mkoa wa Mara ziweze kukamilika kwa wakati.

Ameelezea matumaini yake kuwa baada ya kukamilika kwa barabara hizi zitaenda kuufungua Mkoa wa Mara kimawasiliano na kurahisisha usafiri kwa wananchi.  

Kwa upande wake akizungumza katika ufunguzi wa hafla hiyo Mratibu wa TARURA  Mkoa wa Mara Mhandisi Musa Z. Mzimbiri ameeleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 8 kwa ajili ya kujenga barabara, vivuko na madaraja katika Mkoa wa Mara.

“Serikali pia imetenga zaidi shilingi bilioni 13.4 kwa ajili ya barabara za majimbo 10 ya uchaguzi ya Mkoa wa Mara katika kutekeleza miradi ya barabara za majimbo ya uchaguzi” amesema Mhandisi Mzimbiri.

Mhandisi Mzimbiri ameeleza kuwa miradi ambayo imewekwa saini leo ni miradi 122 inayotekelezwa na wazabuni 34 yenye gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 6.044 katika halmashauri na wilaya zote za Mkoa wa Mara.

Hafla fupi ya kutia saini ya ujenzi wa barabara zinazosimamiwa na TARURA ilihudhuriwa pia na viongozi wa taasisi za kifedha, bima, madini, wakandarasi, maafisa kutoka Ofisi ya Mratibu wa TARURA Mkoa wa Mara na waandishi wa habari.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa