• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Msovela aendelea na ukaguzi wa Miradi

Posted on: November 9th, 2021

MSOVELA AFANYA UKAGUZI WILAYA TATU

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela leo tarehe 6 Novemba 2021 ameendelea na ukaguzi wa miradi kwa kufanya ukaguzi katika Wilaya nne wa ofisi za Maafisa Tarafa na pamoja na miradi miundombinu inayoendelea kujengwa kutokana na fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Akizungumza katika maeneo mbalimbali Bwana Msovela amewakumbusha wasimamizi wa miradi kuwa Mkoa wa Mara umeazimia kukamilisha miradi hiyo tarehe 1 Desemba 2021 ili kuruhusu wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanza masomo kwa wakati.

“Kama Mkuu wa Mkoa alivyoagiza, miradi hii tunapaswa kuikamilisha kabla ya muda uliopangwa na serikali,na hili tukiongeza juhudi inawezekana lengo hilo likatimia kwa wakati” alisema Bwana Msovela.

Katika miundombinu inayojengwa, Bwana Msovela ameshuhudia miundombinu ikiwa katika hatua mbalimbali za kujenga msingi na kuwataka Wasimamizi wa Kata kutoka Halmashauri kwenda kusimamia kwa ukaribu miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati kama ilivyopangwa.

Aidha kutokana na uchakavu wa Ofisi za Maafisa Tarafa, Bwana Msovela aliagiza kuwa fedha za ukarabati wa majengo hayo zitengwe katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 ili yaweze kukarabatiwa.

Aidha alisema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara itaangalia uwezekano wa kununua samani za ofisi na vitendea kazi kwa ajili ya Maafisa Tarafa wa Mkoa mzima.  

Katika ziara hiyo, Bwana Msovela alikagua Ofisi ya Afisa Tarafa ya Suba, Shule ya Sekondari ya Suba, Shule ya Sekondari ya Buturi, Shule ya Sekondari ya Pasta Raphael Odunga na Ofisi ya Afisa Tarafa Luo Imbo katika Wilaya ya Rorya.

Katika Wilaya ya Tarime alikagua Ofisi ya Afisa Tarafa ya Inano na Ofisi ya Afisa Tarafa ya Inchage. Katika Wilaya ya Serengeti Katibu Tawala alitembelea Ofisi ya Afisa Tarafa ya Ikorongo, nyumba iliyojengwa kwa ajili ya Afisa Tarafa ambayo haijapokelewa na Serikali baada ya kujengwa chini ya kiwango, Kituo cha Afya Kenyana na Shule ya Sekondari ya Samoche.

Katika Wilaya ya Butiama, Katibu Tawala alitembelea Ofisi na nyumba ya kuishi Afisa Tarafa ya Kiagata, Shule ya Sekondari ya Bumangi na Ofisi ya Afisa Tarafa ya Makongoro.

Bwana Msovela aliambatana na Kaimu Mhasibu Mkuu wa Mkoa Bwana Pascal Kajuna, Mkaguzi Mkuu wa Ndani Bwana Yusuf Luhende, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi- Miundombinu Mhandisi Richard Moshi, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi- Utawala na Rasilimaliwatu Bwana Dominicus Lusasi na Mwakilishi wa Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara Bwana Fidel Baragaye.

Ziara hiyo ni mwendelezo wa ziara za Katibu Tawala kukagua miradi Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 katika Wilaya zote za Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa