• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mpango wa Serikali kuwa na Shule za Msingi kila Kijiji: Majaliwa

Posted on: February 26th, 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) leo ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Mara ambapo amefanya ziara katika Wilaya ya Bunda na kuzungumzia mpango wa Serikali kuwa na shule ya msingi kila kijiji.

Akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua Shule ya Msingi Kihumbu, Mhe. Majaliwa amesema Serikali inampango pia wa kujenga Shule za Msingi katika vitongoji vyenye watoto wengi ili kupunguza msongamano wa wanafunzi  katika shule hizo.

Mhe. Majaliwa amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Kihumbu kwa kutoa eneo lao bure kwa ajili ya mradu wa ujenzi wa Shule ya Msingi Sabasita na kushiriki katika kusafisha eneo hilo kabla ya ujenzi wa shule hiyo kuanza.  

Akizungumza baada ya kukagua, kutembelea na kupanda mti wa kumbukumbu katika shule hiyo, Mhe. Majaliwa amewataka wananchi kuendelea kutoa michango ya shughuli za maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule, nyumba za walimu, vyoo na kadhalika yenye kibali cha Mkuu wa Wilaya.

Mhe. Waziri Mkuu ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na wasimamizi wa mradi huo kwa kukamilisha mradi kwa wakati, ubora na kubakisha kiasi cha shilingi 221,636 baada ya kukamilisha mradi huo.

Mhe. Waziri Mkuu pia ametumia nafasi hiyo kuwahamasisha wazazi kuwapeleka watoto kuanzia umri wa miaka minne shule ili waweze kujifunza na kuangiza Shule zote hapa nchini kutenga vyumba kwa ajili ya madarasa ya awali ili watoto wadogo wasikae chini ya miti wakati wa kujifunza.

Kwa upande wake, akitoa taarifa ya shule hiyo, Mwalimu Gatrida Malegesi ameeleza kuwa Shule ya Msingi Sabasita imejengwa kwa gharama ya shilingi 348, 000,000 na ujenzi wake umekamilika, imesajiliwa na imeanza kuchukua wanafunzi kuanzia Januari, 2024 na kwa wasasa wanafunzi 345.

Mwalimu Malegesi ameeleza kuwa kati ya wanafunzi waliopo, wasichana ni 169 na wavulana wapo 176 ambao baadhi yao wamepunguzwa kutoka Shule ya Msingi ambayo ilikuwepo katika kijiji hicho na shule hiyo imejengwa ili kupunguza msongamano wa wanafunzi.

Mwalimu Malegesi ameeleza kuwa shule hiyo ni sehemu ya shule zilizojengwa kwa ufadhili wa mradi wa BOOST katika Mkoa wa Mara.  

 Wakati huo huo, Mhe. Waziri Mkuu leo amewasalimia wananchi wa Kijiji cha Mariwanda, ametembelea na kukagua Shule ya Msingi SabaSita, ameweka jiwe la msingi katika Mradi wa ujenzi wa Shule ya Wasichana ya Mkoa wa Mara, amefanya kikao cha ndani na watumishi na kufanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Msingi Miembeni.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa