• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa awahimiza wananchi kushiriki chanjo

Posted on: September 1st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewahimiza wananchi wa Mkoa wa Mara kuhakikisha watoto wote chini ya miaka mitano wanapata chanjo ya ugonjwa wa polio ya matone.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Chanjo ya Polio katika Mkoa wa Mara iliyofanyika katika Kituo cha Afya cha Nyasho, Manispaa ya Musoma, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa ni vizuri watoto wote wapate chanjo ya ugonjwa wa polio.  

“Mtoto asiyepata chanjo ya polio ni hatari kwake yeye mwenyewe na jamii yote inayomzunguka maana wataalamu wanasema ugonjwa huu unaambikiza na mtu akishaupata hautibiki tena” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, amewaagiza wasimamizi wa Sekta ya Afya kuhakikisha kuwa zoezi hili linafanyika vizuri na kwa uaminifu ili Taifa liweze kuwa salama kutokana na uwezekano wa watu kupata ugonjwa wa polio.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Mzee ameipongeza Idara ya Afya ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na wasimamizi wote wa Afya katika ngazi mbalimbali kwa kusimamia vizuri kampeni ya chanjo kwa awamu ya pili na kuuwezesha Mkoa kuvuka lengo la kuchanja kwa asilimia 119.

“Ninawapongeza sana wasimamizi wote wa sekta ya afya na wananchi wa Mkoa wa Mara kwa kazi nzuri iliyofanyika katika awamu ya pili ya chanjo ya polio hapa nchini ambapo Mkoa wetu ulifanya vizuri” alisema Mheshimiwa Mzee.

Kwa upande wake, Meya wa Manispaa ya Musoma Mheshimiwa William Gumbo ameeleza kuwa Manispaa ya Musoma imejipanga vizuri katika kufanikisha kampeni ya chanjo ya polio kwa muda uliopangwa.

“Katika awamu ya pili tulitarajia kutoa chanjo kwa Watoto 37,000 lakini tukavuka lengo na kuchanja Watoto 43,000 ambao ni sawa na ongezeko la asilimia 130 ya lengo la awali” alisema Mheshimiwa Gumbo.

Mheshimiwa Gumbo ameeleza kuwa katika kampeni ya chanjo awamu ya pili, Manispaa hiyo iliwatumia Wenyeviti wa Mitaa ambao tayari Manispaa imeshafanya nao kikao kwa ajili ya kuhamasisha ushiriki wao katika Kampeni ya Chanjo awamu ya tatu.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya Dkt. Juma Mfanga ameeleza kuwa hii ni awamu ya tatu ya Kampeni ya Chanjo ya Polio hapa nchini baada ya mgonjwa wa polio kupatikana katika nchi ya Malawi Februari, 2022.

Dkt. Mfanga ameeleza kuwa baada ya hapo awamu ya kwanza ilikuwa ni katika mikoa inayoizunguka Malawi ambayo ni Mbeya, Njombe, Iringa, Songwe na Ruvuma ambayo ilipata chanjo mwezi Machi, 2022 na awamu ya pili ilifanyika nchi nzima kuanzia Mei 18-22, 2022.

Dkt. Mfanga ameeleza kuwa katika awamu hii ya tatu, kampeni ya chanjo itafanyika nyumba kwa nyumba kama ilivyokuwa katika awamu ya pili na katika kampeni hii hamna namna wataalamu wa afya wanaweza kutoa taarifa za uongo kuhusu chanjo kutokana na mfumo wa ufuatiliaji unaotumika.

Akizungumzia faida za chanjo hiyo, Dkt. Mfanga ameeleza kuwa chanjo hiyo inauwezo wa kukinga ugonjwa wa polio ambao hushambulia mishipa ya fahamu na kumfanya muathirika kupooza na kupata ulemavu wa kudumu.  

Kampeni ya chanjo ya polio imeanza leo tarehe 1 Septemba, 2022 hadi tarehe 4 Septemba, 2022 hapa nchini kwa wataalamu wa afya kupita nyumba hadi nyumba kuchanja watoto wenye chini ya miaka mitano.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa