• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa apokea madarasa 58 Serengeti

Posted on: January 6th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amepokea vyumba vya madarasa 58, viti na meza kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.16 kwa ajili ya madarasa ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023.

Akizungumza baada ya kupokea madarasa hayo, Mheshimiwa Mzee ameipongeza Wilaya ya Serengeti kwa kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa ubora na kwa wakati.

“Ninawapongeza wote waliohusika katika usimamizi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa haya, kazi iliyofanyika ni nzuri na nimeridhika na ujenzi huu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee pia amezipongeza shule ambazo zimepanda miti kuzunguka maeneo yao na kuzitaka shule hizo kuongeza miti zaidi ili kila mwanafunzi aweze kupata mti wake wa kuuhudumia akiwa shuleni hapo.

Hata hivyo, Mheshimiwa Mzee ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kusimamia na kuhakikisha mapungufu madogo madogo yaliyobainika yanaondolewa ili wanafunzi wanapoanza masomo mapungufu hayo yawe yameondolewa.

Mapungufu hayo ni pamoja na ubora wa viti na meza zilizotengenezwa, uingizaji wa umeme katika vyumba vya madarasa, uwekaji wa ngazi katika madarasa hayo na kufanya landscaping katika maeneo ya shule hizo.

Aidha, Mheshimiwa Mzee ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kuongeza vyumba vya madarasa katika shule za sekondari za Mugumu na Rigicha ambazo zilieleza kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa kutokana na uwingi wa wanafunzi katika shule hizo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Dkt. Vincent Mashinji ameeleza kuwa kukamilika kwa vyumba hivyo vya madarasa kutawasaidia wanafunzi zaidi ya 7,000 wanaoanza kidato cha kwanza mwaka huu.

“Kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Serengeti, ninamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za kujenga vyumba 58 vya madarasa katika Wilaya ya Serengeti vimesaidia sana katika maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza” alisema Dkt. Mashinji.

Mheshimiwa Dkt. Mashinji amewataka wazazi wa wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kuhakikisha kuwa wanapeleka watoto wao shule kwa hiari yao, wakishindwa kufanya hivyo, Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kisheria.

Aidha, amewaagiza watendaji wa Vijiji, Mitaa na Kata kuhakikisha wazazi wote wenye watoto wanaotakiwa kwenda shule wanapelekwa shule ili watoto waweze kupata haki yao ya kusoma na kujifunza kulingana na umri wao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Mrobanda Japan Mkoma ameeleza kuwa CCM imefurahishwa na kazi nzuri iliyofanyika ya ujenzi wa madarasa hayo ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya chama hicho.

Mheshimiwa Mrobanda amewataka watendaji wote kuendelea kutekeleza Ilani kwa nguvu ili wananchi waweze kukuelewa na kukipenda Chama cha Mapinduzi na viongozi wake.

Aidha, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa na kutoa nafasi kwa wanafunzi wengi kuweza kusoma.  

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa amekagua Shule ya Sekondari ya Rigicha (vyumba 4), Shule ya Sekondari ya Natta (chumba kimoja), Shule ya Sekondari ya Makundusi (vyumba 3), Shule ya Sekondari Mugumu (vyumba 8) na Shule ya Sekondari ya Mapinduzi (vyumba 10).

Katika ziara hiyo pia, Mkuu wa Mkoa amepata nafasi ya kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Natta na kusikiliza maoni, kero, changamoto zinazowakabili na kuzitolea ufafanuzi na mrejesho.

 Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu, watumishi wengine kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, viongozi wa CCM Wilaya ya Serengeti, Madiwani na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa