• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mhe. Mtambi azindua zoezi la uandikishaji wapiga kura

Posted on: October 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amezindua zoezi la kujiandikisha katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara kwa kujiandikisha katika kituo kilichopo Ofisi ya Kata ya Mkendo, Manispaa ya Musoma.

Akizungumza baada ya kujiandikisha, Mhe. Mtambi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili waweze kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuanzia leo hadi tarehe 20 Oktoba, 2024 kwenye vituo vilivyopo katika maeneo yao.

“Ninawasihi wananchi kujitokeza kujiandikisha ili kutumia fursa hii ya kikatiba kuwachagua viongozi watakaowahudumia na kuwaletea maendeleo katika vijiji, mitaa na vitongoji vyenu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema zoezi la uandikishaji linafanyika kwa muda mfupi sana na hivyo wananchi hawana sababu ya kutokushiriki kujiandikisha ili waweze kushiriki kuchagua na kuchaguliwa kuwa viongozi katika maeneo yao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka ambaye pia amejiandikisha katika kituo hicho amewataka wananchi wa Wilaya ya Musoma kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili kuwawezesha kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Mhe. Chikoka amesema hii ni fursa kwao kujiandikisha ili kuweza kuchagua viongozi na kuchaguliwa kuwa viongozi wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji mbalimbali.

Baada ya kujiandikisha Mhe. Chikoka amekagua zoezi la uandikishaji katika Manispaa ya Musoma na kutembelea maeneo mbalimbali yenye mkusanyiko kwa ajili ya kuwahamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajiwa kufanyika hapa nchini 27 Novemba, 2024 na zoezi la kujiandikisha limeanza leo na mwisho ni tarehe 20 Oktoba, 2024 na sifa za mtu kujiandikisha ni awe raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 au zaidi, mkazi wa mtaa, kijiji au kitongoji ambapo uchaguzi unafanyika.

Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti wa Mtaa, wajumbe wa kamati ya mtaa (kundi mchanganyiko) na kundi la wananwake hii ni kwa Halmashauri za Mji na Manispaa wakati katika Halmashauri za Wilaya nafasi zinazogombewa ni Mwenyejiti wa Kijiji, wenyeviti wa vitongoji vilivyomo katika Kijiji na kundi la wanawake.

Hafla ya uzinduzi imeshuhudiwa na watumishi kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Manispaa ya Musoma pamoja na wananchi waliokuwepo katika eneo hilo.

 Kauli mbiu ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu ni “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze Kushiriki Uchaguzi”.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa