• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Meja Gowele: Jitokezeni kupiga kura

Posted on: November 2nd, 2024

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele amewaongoza maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Mara kushiriki Serengeti Utalii Nyama Choma Festival na kuwahamasisha kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba, 2024.

Akizungumza katika tamasha hilo lililofanyika katika eneo la mnadani, Mjini Mugumu Mhe. Gowele amewataka wananchi waliojiandikisha kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi kwa kupiga kura na kuchagua viongozi wakataowaongoza katika maeneo yao.

“Pamoja na kwamba tumejiandikisha na tumepiga kura ndani ya vyama vya siasa, tusipopiga kura siku ya uchaguzi haitakuwa na maana kwa sababu hatutaweza kuwachagua viongozi tunaowataka watakaotuletea maendeleo katika maeneo yetu” amesema Mhe. Gowele.

Mhe. Gowele amewataka wananchi kushiriki katika kampeni zitakazofanyika ili kuwafahamu wagombea wanaowania nafasi mbalimbali na kujua sera zao kabla ya kupiga kura ili kupata uelewa mpana kuhusu wagombea wanaowania nafasi mbalimbali.

Mhe. Gowele amewataka wananchi kulinda amani na utulivu na hususan wakati huu wa uchaguzi na kuwahakikisha kuwa Serikali itahakikisha kuwa kuna kuwepo amani na utulivu muda wote  na watakaoanzisha uvunjifu wakati huu watachukulia hatua kali za kisheria na kuwataka wananchi kutoa taarifa kwa viongozi kama kuna jambo lolote wamebaini katika maeneo yao.

Aidha, Meja Gowele amewataka wananchi kutunza mazingira katika maeneo yao na kutokomeza ujangili ili kuhifadhi maliasili za Tanzania ili nchi iweze kupata manufaa ya kiuchumi yanayotarajiwa kwa kuhifanyi maliasili hizo zilizopo katika maeneo mbalimbali.  

Mhe. Gowele amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi kwa mawazo yake ya kuanzisha nyama choma festival ambayo inawainua wajasiriamali wadogo wadogo na wachoma nyama waliochangamkia fursa katika Mkoa wa Mara.

Meja Gowele amewahamasisha wajasiriamali kujiunga kwenye vikundi ili waweze kufaidika na mikopo inayotolewa na Halmashauri, Serikali na wadau wengine ili kuboresha biashara zao na hali zao za maisha.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Kemirembe Lwota amewashukuru wananchi wa Serengeti kwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye orodha ya wakazi na kuwahamasisha kushiriki kupiga kura ili kuweza kuwachagua viongozi watakaowaletea maendeleo.

“Ninawasihi tujitokeze kwa wingi, tupige kura ili kupata viongozi bora watakaosimamia maendeleo katika maeneo yetu” amesema Mhe. Lwota.

Mhe. Lwota amewashukuru wadhamini waliofanikisha tamasha hilo kwa michango yao waliyoitoa ili kufanikisha tamasha hilo ambao amewataja kuwa ni Nyansaho Foundation, Grumeti Fund, TAWA, SENAPA, Wanyancha Pub na kadhalika.

Kwa upande wake, Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Nyansaho Foundation Bibi Esther Mng’ori ambao walikuwa wadhamini wakuu wa tamasha hilo ameishukuru ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Serengeti kwa kuwashikirisha katika maandalizi ya tamasha hilo kama wadhamini na washiriki.

Amesema taasisi yao inahusika na utoaji wa huduma na misaada kwa kushirikiana na Serikali katika elimu, afya na watu wenye mahitaji maalum katika Wilaya ya Serengeti.

Tamasha hilo lilianza na mbio na mazoezi ya viungo asubuhi na kufuatiwa na mashindano mbalimbali ya michezo na kuhitimishwa na mashindano ya uchomaji wa nyama na kupambwa na burudani zilizotolewa na wasanii mbalimbali.

Katika tamasha hilo pia, Meja Gowele alitoa zawadi kwa washindi wa mbio, michezo mbalimbali  iliyokuwa inashindaniwa na mashindano ya kuchoma nyama katika tamasha hilo.

Wengine walioshiriki katika tamasha hilo ni Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, baadhi ya Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, taasisi za umma na binafsi na wafanyabiashara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa