• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Masatu afungua kikao cha Tathini ya Elimu Mara

Posted on: June 3rd, 2024

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Dkt. Zabron Masatu, leo amefungua kikao cha tathmini ya utekelezaji wa kazi kwa Wasimamizi wa Elimu Mkoa wa Mara na kuwapongeza kwa kubuni kikao hicho cha kujadili utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Sekta ya Elimu kwa kila robo mwaka.

Akizungumza katika kikao hicho Dkt. Masatu amewataka wasimamizi hao kufanya vikao kama hivyo katika ngazi za Halmashauri na shule zilizopo ili kuboresha elimu katika Mkoa wa Mara.

“Ninaipongeza sana Sehemu ya Elimu kwa kuanzisha vikao vya tathmini ambavyo vinafanyika katika kila robo kwa ngazi ya Mkoa ni jambo zuri na la kuigwa kwa Sehemu na Vitengo vingine katika utekelezjai wa majukumu yao” amesema Dkt. Masatu.

Dkt. Masatu amepongeza kikao hicho kujadili suala la utoaji wa chakula mashuleni ambalo amesema kuwa ni muhimu sana katika utekelezaji wa Mwongozo wa Kitaifa wa utoaji wa Chakula masuleni na mkataba wa lishe wa Kitaifa.

Dkt. Masatu ametaka kuwepo na mipango thabiti ya utekelezaji na usimamizi wa shughuli za elimu na  kuzihusisha sekta nyingine pale inapohitajika.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Bulenga Makwasa ameeleza kuwa Sehemu ya Elimu imeanzisha utaratibu wa kufanya vikao vya tathmini katika kila robo mwaka ili kuinua ubora wa elimu na kuondoa  baadhi ya changamoto zilizokuwa zinakwamisha maendeleo ya elimu.

“Kuanzia  mwaka huu wa fedha wa 2023/2024 tumeanza kufanya tathmini hizi ambazo zinawahusisha Maafisa Elimu wote wa Halmashauri pamoja na wasaidizi wao ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya elimu katika Mkoa wa Mara” amesema Bwana Makwasa.  

Bwana Makwasa amesema katika kikao hicho mambo mbalimbali yatajadiliwa ikiwemo taarifa ya tathmini ya utekelezaji wa KPI katika robo ya pili ya mwaka 2024 ya kila Halmashauri itakayowasilishwa na Maafisa Elimu wa Halmashauri.

Bwana Makwasa amesema jambo linguine litakalojadiliwa ni taarifa ya maandalizi ya Wiki ya Elimu ya Watu Wazima, 2024 ambapo Maafisa Elimu wa Halmashauri watawasilisha maandalizi ya kila Halmashauri.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa