• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yazindua utekelezaji wa anuani za makazi

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amezindua utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuhusu anuani za makazi.

Mheshimiwa Hapi amezindua utekelezaji huo leo katika ukumbi wa uwekezaji ambapo ametoa mwisho wa utekelezaji wa mradi huo kwa Mkoa wa Mara kuwa tarehe 1 Aprili 2022.

“Mheshimiwa Rais katika maelekezo yake amesema mwisho wa kutekeleza jambo hili kitaifa ni tarehe 1 Mei, 2022 lakini sisi kwa Mkoa wa Mara mwisho ni tarehe 1 Aprili 2022 ili kutoa nafasi ya tathmini na kuandaa taarifa ya Mkoa kabla ya tarehe 1 Mei, 2022 alisema Mheshimiwa Hapi.

Mkuu wa Mkoa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa zoezi hilo kila baada ya wiki mbili kuanzia sasa.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa zoezi la uwekaji wa anuani za makazi ni muhimu sana kwa ajili ya utekelezaji wa Sensa ya Watu na Makazi ambayo inategemewa kufanyika mwezi Agosti, 2022 hapa nchini.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali, vibao vya mtaa, vijiji na makazi binafsi serikali haitavitengeneza na badala yake wananchi watatengeneza vibao hivyo wao wenyewe.

Amewataka Wakuu wa Wilaya na Halmashauri kufanya mikutano ya kuwaelimisha wananchi kuhusiana na umuhimu wa zoezi hilo na namna wanavyoweza kushiriki.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa katika utekelezaji wa suala hilo, Wakala wa Barabara (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) wanatakiwa kuweka vibao vya mitaa inayogusana au inayochepuka kutoka barabarani katika barabara zote zinazojengwa sasa hivi au zitakazojengwa kuanzia sasa.

Mheshimiwa Hapi amezitaka Wilaya kuunda kamati maalum za utekelezaji wa zoezi hilo kuanzia ngazi za wilaya hadi katika vijiji na mitaa ili kufanikisha zoezi hilo.

Aidha amezitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa kila mtaa, Kijiji, maeneo ya biashara na makazi ya watu yanakuwa na vibao vya kuyatambulisha vinavyosomeka na kuonekana kiurahisi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa katika kutekeleza zoezi hilo serikali italeta fedha zenye maelekezo kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi hilo, “hazitatumika kama fedha za OC, hizi zitakuwa na maelekezo maalum” alisema Mheshimiwa Hapi.

“Maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuwa Halmashauri zitoe msaada katika zoezi hili kwani zoezi linatakiwa kufanywa na watumishi wa umma na sio watu wa nje ya serikali” alisema Mheshimiwa Hapi. 

Awali, akisoma taarifa kuhusiana na miongozo ya serikali kuhusu anuani za makazi, Kaimu Afisa TEHAMA wa Mkoa Bwana Amon Stephano Mwasambungu ameeleza kuwa katika kutekeleza zoezi hilo  mfumo utakaotumika unasomana na GPS.

“Kwa hivyo baada ya kazi uthamini utafanyika katika ngazi mbalimbali hivyo zoezi linatakiwa kufanywa kwa umakini, uadilifu na ukweli katika ngazi zote” alisema Bwana Mwasambungu.  

Bwana Mwasambungu amezitaka Halmashauri kuwashirikisha Maafisa TEHAMA wa Halmashauri katika Kamati za kutekeleza jukumu hilo ili kufanikisha zoezi hilo kwa ufanisi zaidi.

Aidha, Bwana Mwasambungu amezitaka Halmashauri kutumia miongozo iliyotolewa na Serikali kuhusiana na anuani za makazi na ili kufanikisha zoezi hilo.

Zoezi la uwekaji wa anuani za makazi kitaifa lilianza mwaka 2017 katika baadhi ya mikoa hata hivyo kwa mwaka huu zoezi hilo litafanyika nchi nzima kuanzia tarehe 18 Februari 2022 hadi tarehe 01 Mei, 2022.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa