• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yazindua PTJ-MMAM

Posted on: September 29th, 2023

Mkoa wa Mara leo umezindua rasmi Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMAM) -2021/2022-2025/2026 na kuzitakaa Halmashauri na wadau wote kuweka katika mipango na bajeti masuala muhimu katika utekelezaji wa mpango huo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa program hiyo, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Dkt. Khalfan Haule amezitaka taasisi za umma, dini na mashirika yasiyo ya kiserikali kushirikiana katika kutekeleza programu hiyo.

“Serikali inaamini kuwa msingi mzuri wa watoto unajengwa katika miaka ya awali ambayo ni 0-8 na baada ya hapo kumbadili mtoto ambaye hakupata malezi stahiki inakuwa ni vigumu sana, kwa hiyo tushirikiane kuwatunza watoto” amesema Mhe. Haule.

Aidha, Dkt. Haule amezitaka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuzindua Programu hiyo katika ngazi ya Halmashauri kabla ya tarehe 30 Novemba, 2023 na kuwataka Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia utekelezaji wa Programu hii katika Halmashauri zao.  

Dkt. Haule amesema maeneo makubwa matano ambayo yamepewa kipaumbele katika programu hii ni pamoja na lishe bora, afya bora, malezi yenye mwitikio, ulinzi na usalama wa mtoto na fursa ya ujifunzaji wa awali.   

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Marco Maduhu amewashukuru viongozi wa dini na mashirika yasiyo ya kiserikali kwa kuitikia wito na kuhudhuria katika uzinduzi huo.

Aidha, Bwana Maduhu ameahidi kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Mkuu wa Mkoa kuhusiana na programu hiyo katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Aidha, Bwana Maduhu amewaomba viongozi wa dini na mashirika yasiyo ya kiserikali kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha kuwa watoto wanalelewa katika mazingira mazuri na kuhakikishiwa usalama wao.

Bwana Maduhu amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuwekeza katika malezi, makuzi na maendeleo ya watoto lakini ili kufanikisha hilo ushiriki wa wadau wa maendeleo ni muhimu sana.

 Uzinduzi wa program hiyo umehudhuriwa pia na Bibi Agness Mbiu mwakilishi wa Wizara ya Afya, Bibi Mariam Luka Mwakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Programu ya PJT MMAM imezinduliwa kitaifa mwaka jana ikiwa na kauli mbiu ya Mtoto Kwanza inategemea kuunganisha jitihada zilizokuwa zinafanywa na taasisi mbalimbali kwa ajili ya malezi, makuzi na maendeleo ya mtoto kuanzia miaka 0-8.

Kwa Mkoa wa Mara program hii inatekelezwa chini ya uratibu wa kanisa la African Inland Church of Tanzania (AICT) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara.

Wengine waliohudhuria uzinduzi huo ni pamoja na Madawati ya Jinsia ya Jeshi la Polisi, mashirika yasiyo ya kiserikali, vyama vya watu wenye ulemavu na viongozi wa dini.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa