• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaweka mikakati ya kuinua ufaulu

Posted on: July 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhehsimiwa Ally Salum Hapi ameelezea mikakati ya Mkoa wa Mara yenye lengo la kuinua ufaulu wa wanafunzi katika mitahani ya kitaifa.

Mheshimiwa Hapi ameelezea mikakati hiyo leo tarehe 16 Julai 2021 wakati akipokea msaada wa vifaa vya elimu na afya uliotolewa na Benki ya NMB katika Shule ya Msingi Buhare iliyopo katika Manispaa ya Musoma.

“Mpango wa Mkoa ni kuhakikisha kuwa Mkoa wa Mara unashika nafasi ya tatu katika ufaulu wa mitihani ya kitaifa ya darasa la saba, kidato cha pili pamoja na kidato cha nne kwa mwaka 2021” alisema Mheshimiwa Hapi.

Ameeleza kuwa kutokana na ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha sita mwaka huu kwenye matokeo yaliyotangazwa hivi karibuni, Mkoa wa Mara umeshika nafasi ya tatu kitaifa lakini mkoa umejiwekea lengo la kushika nafasi hiyo katika mitihani iliyobakia.

“Kuna kazi ya kufanya kwa sababu ufaulu wa wanafunzi wa shule ya msingi na kidato cha nne sio mzuri sana, walimu wasibweteke na Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara amepewa jukumu kusimamia mikakati yetu ya Mkoa ili iweze kutekelezwa ipasavyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

“Msaada huu wa leo umekuja kutuongezea nguvu katika malengo yetu makubwa ya kukahikisha tunaifikia ndoto hii” alisema Mheshimiwa Hapi

Aidha amemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kuajiri walimu 6,000 na wengi wao wakiwa wa sayansi utaenda kupunguza tatizo kubwa la walimu hapa nchini.

Ameeleza kuwa Mkoa unachukua hatua mbalimbali kuhakikisha walimu wanafundisha wanafunzi madarasani na kuboresha usimamizi mzima wa elimu ili kuinua ufaulu wa wanafunzi.  

Mheshimiwa Hapi amewataka wakurugenzi na maafisa utumishi wa Mkoa wa Mara kusikiliza kero za walimu katika maeneo yao ili kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu kwa wakati.

Aidha amewataka walimu kutimiza wajibu wao ikiwa ni pamoja na kuongeza juhudi katika ufundishaji, usimamizi wa utoro wa wanafunzi na kuwalea wanafunzi wawapo shuleni.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa Mkoa unampango wa kuweka vigezo vitakavyotumika kuwapima walimu wakuu na wakuu wa shule katika kuongeza ufaulu wa wanafunzi katika Mkoa wa Mara.

“Mwalimu Mkuu tutamwekea vigezo vya kumpima ambavyo ni pamoja na ufaulu wa wanafunzi, usimamizi wa masuala ya taaluma, nidhamu na utunzaji wa mali na mazingira ya shule” alisema Mheshimiwa Hapi.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Musoma Mheshimiwa William Gumbo ameeleza kuwa Shule ya Msingi Buhare ambayo imepatiwa msaada na NMB ina changamoto kubwa ya mlundikano wa wanafunzi.

“Kwa sasa shule hii inawanafunzi zaidi ya 1,700 ambao wanafundishwa katika madarasa 22 yaliyopo katika shule hii na hamna eneo la ziada la kuongeza madarasa hapa” alisema Mheshimiwa Gumbo.

Mheshimiwa Gumbo ameeleza kuwa ili kukabiliana na changamoto hiyo tayari Manispaa ya Musoma kwa kushirikiana na wadau wametafuta eneo la kujenga shule mpya ili kupanua miundombinu ya shule na msaada uliopatikana utatumika katika ujenzi wa shule hiyo.

“Tunashukuru kwa msaada huu wa mabati 300 ambayo yatatumika katika kuanza kujenga shule ya msingi mpya ambayo itapunguza msongamano wa wanafunzi katika shule ya Msingi Buhare” alisema Mheshimiwa Gumbo.

Mheshimiwa Gumbo ameeleza kuwa baada ya eneo la kujenga shule kupatikana, Diwani wa Kata ya Buhare na wadau wengine wamechangia mifuko 85 ya saruji na wiki ijayo wanampango wa kukutana na wadau wengine kwa ajili ya kuchangisha fedha za ujenzi wa shule hiyo.

Katika hafla hiyo ya kupokea msaada, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Alfany Haule, Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara Bwana Benjamin Oganga na Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, viongozi wa CCM, walimu na wanafunzi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa