• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yatoa mafunzo ya Magonjwa ya Mlipuko

Posted on: March 19th, 2020

Mkoa wa Mara leo tarehe 17 Machi 2020 umetoa mafunzo kwa watumishi wa afya na sekta zinazohudumia wageni ili kuwajengea uwezo wa kukabiliana na magonjwa ya milipuko ikiwemo yanayotokana na virusi vya Corona (COVID 19) yaliyofanyika katika Chuo cha Matabibu Musoma kilichopo katika Manispaa ya Musoma.  

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dkt. Florian Tinuga amesema lengo la mafunzo hayo ni kujengeana uwezo wa namna bora ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko husuni yanayotokana na vizuri vya Corona.

“Tunataka mafunzo haya yawe ndio msingi wa kukabiliana na dharura zote za afya katika Mkoa wa Mara na matokeo ya mafunzo ni kupata ujuzi na kuandaa timu za kukabiliana na magonjwa ya mlipuko”alisema Dkt. Tinuga.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Method B. Mkoba amewataka watumishi wote wanaopewa mafunzo kuzingatia mafunzo hayo ili wakayatekeleze kwa vitendo.

“Ninyi ndio askari wetu tunaowategemea katika vita hii, mnatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu kwa watumishi wenzenu na wananchi kwa ujumla” alisema Bwana Mkoba.

Aidha amewatoa hofu wananchi wote kuwa Mkoa wa Mara kwa sasa ni salama na kuwasistiza wananchi kufuatilia maelekezo yanayotolewa mara kwa mara na serikali katika kukabiliana na mlipuko wa Corona hapa nchini.  

Bwana Mkoba pia ameipongeza Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake, Wazee na Watoto kwa kazi nzuri inayoendelea kufanya mpaka sasa tangu mlipuko huu ulipotokea.

“Kazi wanayoifanya ni kubwa sana, hususan ya kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu nini kinachoendelea na tahadhari za kuchukua”.

Wakati huo huo Mtaalamu wa Magonjwa ya Mlipuko Dkt. William Nangi ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana hasa kwa mikoa iliyopembezoni kama Mkoa wa Mara ambayo ni rahisi kuambukizwa na watu wanaotokea nje na ndani ya nchi.

“Sisi tunawaandaa ili wawe na utayari wa kuwapokea na kuwahudumia wagonjwa wa milipuko ikiwemo magonjwa yanayotokana na virusi vya Corona” alisema Dk. Nangi.

Mafunzo hayo yanaendeshwa na wataalamu kutoka Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee, Wanawake na Watoto na kuhudhuriwa na viongozi wa afya wa kila wilaya na Halmashauri, wataalamu wa afya kutoka Uwanja wa Ndege Musoma, mpaka wa Tanzania na Kenya wa Sirari, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na vituo vilivyotengwa kwa ajili ya kupokea wagonjwa wa milipuko katika Mkoa wa Mara pamoja na wadau wengine.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa