• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaomba JKT kuongeza Uwekezaji katika Shamba Darasa la Mkoa

Posted on: December 17th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameliomba Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kuwekeza zaidi katika Shamba Darasa la Mkoa wa Mara maarufu kama viwanja vya Mama Maria Nyerere vilivyopo katika Kijiji cha Butiama, Wilaya ya Butiama.

Mheshimiwa Malima ametoa ombi hilo leo tarehe 16 Desemba 2020 ofisini kwake baada ya kumpokea Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Charles Mbuge ofisini kwake akiwa katika ziara ya kutembelea Mkoa wa Mara.

“Kwa Mkoa wa Mara tungefurahi sana kama jeshi letu lingewekeza zaidi katika eneo tulilowatengea katika viwanja vya Mama Maria Nyerere ili wananchi wa Mkoa wa Mara waweze kujifunza na kufaidika na utaalamu wa kilimo uliopo JKT” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima amesema kuwa Mkoa uliamua kuanzisha shamba hilo ili kuweza kuwafikia wakulima wake kiurahisi zaidi katika kuwapa elimu, teknolojia na mifano ya kilimo bora kutoka kwa wataalamu na wakulima waliofanikiwa.

“Bado tunaendelea kushiriki katika maonyesho yanayofanyika katika viwanja vya maonyesho ya kilimo kwa Kanda ya Ziwa Mashariki kule Nyakabindi, Simiyu lakini shamba hili ni fursa kubwa zaidi kwa wakulima wetu maana hapa ni karibu na wanaweza kufika na kujifunza” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha amemshukuru Mkuu huyo kwa kazi kubwa ambayo JKT inaifanya katika kuhamasisha kilimo cha mazao ya kimkakati na hususan kahawa, pamba na mihogo katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake Meja Jenerali Mbugi ameeleza kuwa JKT kwa sasa imewekeza sana katika kilimo cha mazao mbalimbali hapa nchini na kwa sasa imeajiri watu sita ambao ni raia waliobobea katika utaalamu wa kilimo. 

“Tumepata mafanikio makubwa sana kutokana na uwekezaji katika kilimo na kuliwezesha jeshi kununua magari 27 na matrekta 10 kutokana na fedha za ndani” alisema Mkuu wa JKT.

Alisema kwa mwaka huu, JKT imewekeza zaidi katika kilimo katika mikoa na mazao mbalimbali ili kuweza kutoa mafunzo ya kilimo kwa wakulima na kuongeza mapato ya ndani ya jeshi hilo.

Ameahidi kuwa JKT itaongeza uwekezaji wake katika eneo walilopewa katika viwanja hivyo ili kutoa mafunzo kwa wakulima na kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mkoa wa Mara umeanzisha maonyesho ya kilimo katika viwanja vya Mama Maria Nyerere kuanzia mwaka huu ili kutoa mafunzo endelevu kwa wakulima kuhusu mazao ya kimkakati ya chakula na biashara ili kuongeza tija kwa wakulima wake.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa