• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yang'ara matokeo ya kidato cha sita

Posted on: July 21st, 2023

Mkoa wa Mara umepata ufaulu wa asilimia 100 katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha sita kwa mwaka 2023 yaliyotangazwa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) hivi karibuni.

Akizungumza katika kikao cha Menejimenti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kaimu Katibu Tawala sehemu ya Elimu na Ufundi Bwana Makwasa Bulenga ameeleza kuwa kwa mwaka 2023 Mkoa wa Mara umeongeza ufaulu kwa asilimia 0.9 kutoka ufaulu wa asilimia 99.1 wa mwaka 2022.

“Kati ya wanafunzi wote 3091 waliofanya mtihani katika Shule za Sekondari 28, wanafunzi 3090 wamepata daraja la kwanza hadi la tatu na mwanafunzi mmoja tu amepata daraja la nne na hivyo wote wamefaulu” amesema Bwana Bulenga.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa katika Shule ya Sekondari ya Bunda wanafunzi 121 walipata daraja la kwanza ambao ni asilimia 95 ya wanafunzi wote 126 waliofanya mtihani katika shule hiyo na kufanikiwa kupata GPA ya 1.7143 na kushika nafasi ya kwanza katika Mkoa wa Mara.

Aidha, Bwana Bulenga ameeleza kuwa kwa mujibu wa matokeo hayo, Shule za Sekondari ya Bunda na Natta zimefanya vizuri na kufanikiwa kuingia kwenye kumi bora kitaifa katika makundi yao.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa Shule ya Sekondari ya Tarime imeongoza Kitaifa kwa kuwa na wanafunzi wengi waliopata ufaulu wa daraja la kwanza ambapo jumla ya watahiniwa 357 walipata daraja la kwanza kati ya wanafunzi 498 waliofanya mtihani katika shule hiyo.

 “Katika Shule za Sekondari za Natta, Songe na Buturi wanafunzi wake wote waliofanya mtihani huo wamepata daraja la kwanza na la pili tu” amesema Bwana Bulenga.

Akifafanua kuhusu watahiniwa hao, Bwana Bulenga ameeleza kuwa asilimia 55 ya watahiniwa hao walichaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2021 wakiwa na ufaulu wa daraja la tatu na katika matokeo ya kidato cha sita wamepata daraja la kwanza na la pili.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa ufaulu huo ni matokeo ya mkakati maalum wa Mkoa wa Mara wa kutokomeza daraja la nne na sifuri katika ufaulu wa mitihani ya Taifa.  

Bwana Bulenga ameeleza kuwa katika Shule ya Sekondari ya Bunda wanafunzi 121 walipata daraja la kwanza ambao ni asilimia 95 ya wanafunzi wote 126 waliofanya mtihani huo na kufanikiwa kupata GPA ya 1.7143 na kushika nafasi ya kwanza katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Menejimenti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara imeipongeza Sehemu ya Elimu na Ufundi, Halmashauri, Walimu na wanafunzi waliofanya mtihani huo kwa jitihada zao zilizowezesha kupata matokeo mazuri katika mtihani huo.

Aidha, Menejimenti imeitaka Sehemu ya Elimu na Ufundi kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya elimu katika Mkoa wa Mara kuendeleza ufaulu huo kwenye matokeo ya mitihani ya Taifa ya shule ya msingi, kidato cha pili na cha nne.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa