• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yakopea Mbio za Mwenge wa Uhuru

Posted on: June 23rd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Allu Salum Hapi leo tarehe 22 Juni 2021 amepokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika Sekondari ya Robanda iliyopo katika Kijiji cha Robanda katika Pori la Akiba la Ikilongo pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Akizungumza wakati wa kupokea Mwenge wa Uhuru Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa Mkoani Mara utatembele, Kuzindua na kuweka jiwe la msingi katika miradi ya maendeleo 50 na kuwasha Mwenge wa Mwitongo nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

“Mkoa wa Mara ndio mwasisi wa Mwenge wa Uhuru kupitia Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa hivyo leo Mwenge wa Uhuru umerudi nyumbani” alisema Mheshimiwa Hapi.

Baada ya mapokezi hay, Mheshimiwa Hapi aliukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Dkt. Vincent Mashinji na kuanza kuukimbiza katika Wilaya ya Serengeti.

Ukiwa katika Wilaya ya Serengeti, Mwenge wa Uhuru umezindua  mradi wa maji katika Shule ya Sekondari Robanda;  umeweka  jiwe la msingi katika mradi wa lambo la mifugo;  umezindua  ofisi ya Kijiji cha Park Nyigoti; umefungua zahanati ya kijiji cha Koreri; pamoja na kutembelea kitalu cha miche na kuzindua klabu ya mapambano dhidi ya rushwa katika Shule ya Sekondari ya Kitunguruma.

Aidha Mwenge wa Uhuru  umefungua Kituo kidogo cha Polisi cha stendi mpya ya Mugumu; umekagua mfumo wa kielektroniki wa ukusanyaji wa mapato ya hospitali (GOTHOMIS) katika Hospitali ya Nyerere (DDH) na umetembelea mradi wa barabara ya lami na kukagua shughuli za vijana zinazofanywa na  kikundi cha Bloom Youth Group mjini Mgumu.

Hata hivyo Mwenge wa Uhuru umeukataa mradi wa ujenzi wa bwalo la chakula katika Shule ya Sekondari ya Robanda kutokana na mapungufu mbalimbalimbali.

Kauli mbiu ya mbio maalum za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu “TEHAMA ni Msingi wa Taifa Endelevu: Itumike kwa Usahihi na Uwajibikaji.

Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizinduliwa tarehe 17 Mei 2021 katika Mkoa wa Kusini Unguja  na kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Wiki ya Vijana Kitaifa 2021 itafanyika mkoani Geita tarehe 14 Oktoba 2021.

Katika Mkoa wa Mara Mwenge wa Uhuru unakimbizwa kuanzia leo hadi tarehe 27 Juni 2021 na tarehe 28 Juni 2021 utakabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa