• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yajipanga kupokea wageni

Posted on: February 1st, 2022

Mkoa wa Mara umejipanga kuwapokea wageni mbalimbali watakaokuja kushiriki kilele cha maadhimisho ya miaka 45 ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ziara ya Mheshimiwa Rais kuanzia tarehe 4-7 Februari, 2022.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ametoa kauli hizo leo tarehe 1 Februari, 2022 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Mkoa unatarajia kupokea wageni takriban 5,000 katika kipindi hiki na niwahakikishie watapata huduma za malazi, usafiri, mawasiliano na mahitaji mengine muhimu wakati wote wakiwa Mara” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewahakikishia watanzania kuwa tayari uongozi wa Mkoa wa Mara umefanya mazungumzo na wafanyabiashara mbalimbali wanaotoa huduma na kuwataka watoe huduma kwa weredi, usafi na viwango vinavyokubalika wakati huu.

“Tumeamua katika kipindi hiki chote baa, kumbi za starehe na sehemu za chakula zitanyakazi kwa masaa 24 ili kuwawezesha wageni kupata huduma kiurahisi zaidi wakati wote wanapohitaji” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara kutumia fursa hii kikamilifu ili kuweza kujitangaza na kujiimarisha katika biashara zao na hususan biashara za huduma mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, amewahakikishia wageni wote kuwa Mkoa wa Mara upo salama siku zote na wakati wote wa ziara ya Mshehimiwa Rais itafanyika kwa utulivu na amani.

Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuwasaidia wageni mbalimbali watakaohitaji kujua kuhusiana na maeneo muhimu na sehemu za kupata huduma mbalimbali.  

“Mimi ninajua kuwa wananchi wa Mkoa wa Mara ni wakarimu na wanapenda sana wageni hivyo sina mashaka kwamba wageni watapokelewa vizuri katika ziara hiyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi amewahimiza wananchi wote kuishi kwa amani, upendo na utulivu wakati wote ambapo Mkoa una wageni ili wageni wakalitangaze vyema jina la Mkoa wa Mara huko waendako.   

 Wageni wanaotarajia kushiriki ziara hii ya Mheshimiwa Rais ni pamoja na Viongozi Wakuu wa Kitaifa, Viongozi wa Kitaifa waliostaafu, viongozi na makada wa Chama cha Mapinduzi, Wabunge, Viongozi mbalimbali wa Serikali, wafanyabiashara, wanachama wa CCM na wananchi wa kawaida.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa