• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yajadili Mpango Mkakati wa Chakula Shuleni

Posted on: September 23rd, 2020

MARA YAJADILI MPANGO MKAKATI WA CHAKULA SHULENI 

Wadau wa elimu wa Mkoa wa Mara leo tarehe 23 Septemba 2020 wamejadili rasimu ya Mpango Mkakati wa Chakula na Lishe Shuleni Mkoa wa Mara wenye lengo la kuboresha taaluma, kuinua ufaulu na afya za wanafunzi.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha wadau wa kujadili rasimu ya mpango huo, mgeni rasmi katika ufunguzi wa kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mheshimiwa Dkt. Vincent Anney Naano amewahimiza wajumbe kuchangia rasimu hiyo ili kupata mkakati mzuri.

“Mara ni mkoa wa kwanza kuandaa Mpango Mkakati wa Chakula na Lishe Shuleni, kwa hiyo mpango huu utatumika na mikoa mingine kama rejea watakapokuwa wanaandaa mipango yao, hivyo ni vizuri tuutendee haki kwa kuchangia maoni yetu na baadae wataalamu watayafanyia kazi” alisema Mheshimiwa Naano.

Mheshimiwa Naano ameeleza kuwa Mpango Mkakati wa Chakula na Lishe Shuleni unatokana na kikao cha wadau cha kujadili changamoto za elimu katika Mkoa wa Mara kilichafanyika tarehe 23 Februari 2020 ambapo uliazimia kuanzisha mpango wa chakula mashuleni.

“Katika mkutano ule, tafiti mbalimbali za changamoto za elimu zilizofanywa katika Mkoa wa Mara zilionyesha kuwa chakula kilikuwa ni moja ya vitu muhimu vya kupewa kipaumbele katika uboreshaji wa elimu katika Mkoa wa Mara”.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi Karoline Mthapula amesema kuwa chakula mashuleni kitaboresha afya na lishe za wanafunzi, itasaidia kuongeza mahudhurio, uandikishaji na usikivu wa wanafunzi darasani.

“Kwa zile shule ambazo chakula kinatolewa shuleni, wanafunzi wamekuwa wakifanya vizuri ukilinganisha na shule ambazo hazina chakula kabisa” alisema Bibi Mthapula.

Aidha amelipongeza Shirika la Project Concern International (PCI) Tanzania kwa kazi kubwa wanayoifanya katika Mkoa wa Mara hususan katika utoaji wa chakula katika baadhi ya shule zinazofikiwa na mradi wa Chakula Shuleni.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miradi wa PCI Tanzania Bi. Amina Mgeni amesema shirika la PCI limekuwa likifanyakazi na Halmashauri nne za Mkoa wa Mara ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Halmashauri ya Mji wa Bunda, Halmashauri ya Musoma Vijijini na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Bi. Mgeni ameeleza kuwa mpango mkakati huu unalenga kutoa mwongozo wa uzalishaji na uchangiaji wa chakula kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

 Mkutano wa kujadili rasimu ya Mpango Mkakati wa Chakula na Lishe Shuleni katika Mkoa wa Mara umehudhuriwa na wataalamu na viongozi wa serikali, viongozi wa dini, wanafunzi, walimu na watumishi wa PCI na mashirika yasiyo ya kiserikali.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa