• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yajadili kuanza kwa Mradi wa MJNUAT

Posted on: November 14th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee, leo ameongoza warsha ya wadau kutambulisha mradi wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknlojia (MJNUAT) baada ya kupokea mkopo wa masharti nafuu shilingi bilioni 102.3 kutoka Benki ya Dunia.

Akizungumza katika kikao hicho Mheshimiwa Mzee amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotokana na kuanzishwa kwa Chuo hicho cha kwanza cha umma katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

“Mimi ninaamini Chuo hiki kitachagiza maendeleo ya Mkoa wa Mara, wito wangu ni wananchi wa Mkoa wa Mara kuchangamkia fursa za kuanzishwa kwa Chuo hiki katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewataka watendaji na viongozi wote watakaohusika katika ujenzi huo kuzingatia uadilifu, weredi na mradi kukamilika kwa wakati ili manufaa ya mradi huu yaonekane mapema.

Mheshimiwa Mzee amewataka viongozi katika maeneo mbalimbali kuwaelimisha wananchi kuhusiana na fursa zilizopo kutokana na kuanzishwa kwa Chuo hicho ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa nafasi za mafunzo ya elimu ya juu ili wananchi nao waweze kuchukua hatua za maksudi kuboresha shughuli mbalimbali.

Ameahidi kuwasimamia watendaji na viongozi wote wa Mkoa wa Mara kutatua changamoto zote zinazoweza kukkwamisha utekelezaji wa mradi huo katika hatua mbalimbali.  

Kwa upande wake Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Lesakit Mellau ameeleza kuwa lengo la Serikali kuanzisha Chuo cha MJNUAT hicho ni kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Makao Makuu ya Chuo hicho yatakuwa katika Wilaya ya Butiama.

Prof. Mellau ameeleza kuwa mpaka sasa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari amemteua Mheshimiwa Peter Pinda, Waziri Mkuu Msaatafu kuwa Mkuu wa Chuo hicho na Katibu Mkuu Kiongozi Mtaafu Bwana Philemon Luhanjo kuwa mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho.

Prof. Mellau ameeleza kuwa katika mradi wa ujenzi unaoanza sasa, ujenzi utafanyika katika maeneo mawili, Kampasi kuu ambayo inatarajiwa kufanyika katika Wilaya ya Butiama na Kampasi ya Tabora ambayo inatarajiwa kujengwa katika Mkoa wa Tabora.

“Hii inatokana na maamuzi ya Serikali ya kuvitaka Vyuo vikuu vya Umma kuanzisha Kampasi katika mikoa mbalimbali na kwa Chuo chetu Kampasi itajengwa Tabora ambayo itakuwa na majengo 7 kati ya majengo 28 yanayojengwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia” alisema Prof. Mellau.

Prof. Mellau ameeleza kuwa ujenzi wa awamu hii ukikamilika, Chuo kitaweza kudahili wanafunzi 6,000 na kitakuwa na watumishi wa Chuo zaidi ya 1,000 ambalo amesema litakuwa ni ongezeko kubwa sana la watu katika Mkoa wa Mara.

Prof. Mellau ameeleza kuwa tayari Chuo hicho kimeandika miradi mbalimbali na ikifadhiliwa yote Chuo kitakuwa na miundombinu ya kutosha ili kudahili wanafunzi 15,000 katika Kampasi mbalimbali za Mkoa wa Mara na Tabora.

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Fedha, Mipango na Utawala Prof. Msafiri Jackson ameeleza kuwa ujenzi huo utahusisha ndaki ya Kilimo, Shule ya Uhandisi na Teknolojia, Shule ya Uhandisi na Teknolojia Nishati na Madini, Shule Kuu ya Tehama na Biashara, jengo la Utawala, Maktaba, mabwalo mawili ya chakula, viwanja vya michezo, barabara na mabweni yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 2,220.

Prof. Jackson ameeleza kuwa mradi huo ni wa miaka mitano ukijumuisha ujenzi wa miundombinu, mafunzo kwa watumishi na tafiti mbalimbali na kuongeza kuwa ujenzi umeanza, mafunzo kwa watumishi yanaendelea na tafiti zimeanza tarari zimeanza kufanyika.

“Changamoto kubwa tutakayokutana nayo ni uhaba wa mabweni ya wanafunzi na nyumba za watumishi, kituo cha polisi, kituo cha kutolea huduma za afya, barabara, hoteli na kadhalika.

Kikao kilihudhuriwa na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Kamatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na taasisi za serikali.

Wengine ni wazee mashuhuri, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa kimila, wafanyabiashara na wawekezaji wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa