• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaimarisha Kituo cha Forodha Sirari

Posted on: May 26th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amekagua Kituo cha Forodha Sirari leo tarehe 19 Mei 2020 na kusisitiza kuhusu maagizo aliyoyatoa awali kuhusiana na hatua mpya za kudhibiti ugonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona yaani COVID 19.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa katika maelekezo aliyoyatoa magari na abiria wote kutoka katika nchi ya Kenya hawataruhusiwa kuingia Tanzania kwa sababu ya kudhibiti maambikizi ya Corona katika nchi hizi mbili.

“Kama nilivyoelekeza awali, maagizo yangu hayajabadilika, utaratibu wetu utaendelea kama kawaida hadi hapo nitakapoelekeza vinginevyo” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima alisema kuwa ziara hiyo imekuja baada ya kupokea taarifa kuwa kuna magari ya Kenya matano yaliyoingia nchini kupitia mpaka huo kinyume na maagizo yake jambo ambalo amehakikisha kuwa halikuwa sahihi.

Msheshimiwa Malima amewakumbusha maafisa wa mpaka huo kuwa magari yote kutoka nchi ya Kenya yanaishia mpakani na anayehitaji mzigo uliobebwa ataufuata hapo ili kudhibiti maambukizi ya Corona.

Ameeleza kuwa tangu ugonjwa wa corona umeanza, Mkoa wote wa Mara umekuwa na wagonjwa watano ambao wote walitokea katika Mkoa wa Dar es Salaam na kati ya hao mmoja alifariki lakini wengine wanne wamepona na wanaendelea kufanya shughuli zao.

“Ninashangazwa majirani zetu wanaposema sisi ndio tunawaletea ugonjwa wa Corona jambo ambalo sio sahihi” alisema Malima.

Aidha alieleza kusikitishwa kwake na baadhi ya hatua zinazochukuliwa na nchi ya Kenya hususan kutangaza watanzania wenye Corona na kuamua kufunga mpaka jambo ambalo amesema huenda halijatazamwa vizuri.   

 Katika ziara hiyo Mheshimiwa Malima aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi Karolina Mthapula, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Eng. Mtemi Msafiri na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa