• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yadhibiti mpaka na Kenya

Posted on: May 6th, 2020

Serikali ya Mkoa wa Mara imeimarisha mpaka wa Tanzania na Kenya katika vijiji 14 vilivyopo katika wilaya za Tarime na Rorya ili kudhibiti maambikizi ya ugonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza hayo baada ya kupokea msaada kutoka katika Hoteli ya Kitalii ya Grumeti ya sare na buti za jeshi la akiba pea 100 na vipama joto 15 ili kuunga jitihada za Mkoa katika kupambana na Corona.

“Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara katika vikao vyake na baada ya ziara waliofanya ya kukagua mpaka wa Tanzania na Kenya katika Wilaya za Tarime na Rorya iliamua kuweka Jeshi la Akiba ili liweze kusaidia katika kudhibiti mapambano ya watu wanaoingia Tanzania kupitia vichororo vilivyopo mpakani” alisema Mheshimiwa Malima.

Mhehsimiwa Malima ameeleza kuwa pamoja na askari hao wa Jeshi la Akiba, Mkoa pia umefufua magari machakavu 14 ili yaweze kutumika katika mpango huu maalum wa kuzuia uingiaji holela wa watu kutoka Kenya pasipo kupita katika mipaka rasmi ya nchi.

Alisema kuwa mpaka huo una urefu wa zaidi ya mita 130 na una vijiji 14 ambavyo vyote vina sehemu mbili, sehemu ya Tanzania na sehemu ya Kenya katika kila kijiji. Aidha alisema kuna vichochoro vingi sana na wahalifu na watu wasiofuata sheria wanavuka mpaka kwa kutumia magari binafsi, pikipiki na baiskeli kupitia vichochoro hivyo. 

“Kwa kuimarisha mpaka huu, sio tu tutadhibiti Corona lakini pia tutadhibiti magendo na vitendo vyote visivyofaa katika mpaka huo” alisema Malima.

Msaada huu umekuja wakati muafaka, hususan wakati huu ambapo tunapambana na virusi vya Corona” alisema Mheshimiwa Malima.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Hoteli ya Grumeti Bwana David Nicholaus Mwakipesile ameeleza kuwa lengo la msaada huo ni kuunga mkono juhudi za mkoa katika kupambana na virusi vya Corona.

“Sisi kama Grumeti tunaunga mkono juhudi kubwa inayofanya na serikali ya Mkoa na tunaamini Mkoa wa Mara ukiwa salama, na sisi tutakuwa salama na tutapata wateja” alisema Bwana Mwakipesile.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mara Dkt. Florian Tinuga amewashukuru sana Grumeti kwa msaada huo na utausaidia sana Mkoa kudhibiti maambukizi ya Corona.

“Ninawashukuru sana kwa msaada huu na msaada mwingine wa kutoa elimu kwa wananchi wa Wilaya ya Serengeti” alisema Dkt. Tinuga.

Katika mpango huo, Jeshi la akiba litaungana na vikosi vya uhamiaji, polisi na Mamlaka ya Mapato Tanzania katika kudhibiti mpaka huo katika kipindi hiki ambacho Tanzania inapambana na kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa corona.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa