• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaazimia kuwa kinara wa masuala ya lishe

Posted on: May 19th, 2021

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Mhandisi Faustine Tarai amewataka wajumbe wa Kamati ya Lishe ya Mkoa wa Mara kuhakikisha kuwa Mkoa huu unakuwa katika kumi bora katika utekelezaji wa afua za lishe kitaifa kwa mwaka 2021.

Mhandisi Tarai ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao cha Kamati ya Lishe ya Mkoa wa Mara kilichofanyika leo tarehe 18 Mei, 2021 katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Ninaomba wajumbe na wataalamu mliopo hapa tujitahidi ili tuweze kufika katika kumi bora kwa mwaka huu na baadaye tuboreshe zaidi hadi kufikia kuwa wa kwanza kitaifa” alisema Mhandisi Tarai.

Aidha amemtaka Mganga Mkuu wa Mkoa na wataalamu wengine kurekebisha mapungufu yanayojitokeza katika kadi alama lishe kwa kipindi cha nusu mwaka kuanzia Julai hadi Desemba 2021 ili wakati wa tathmini Mkoa uweze kupata nafasi nzuri zaidi.

Aidha amewataka wataalamu wa Lishe kutekeleza majukumu yao kikamilifu na pale wanapokwama kuomba msaada kwa watendaji wengine ili kuweza kuleta ufanisi katika utekelezaji wa masuala ya lishe hususan kwa wajawazito na watoto.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha Kaimu Katibu Tawala, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya Dkt. Florian Tinuga ameeleza kuwa katika miaka ya hivi karibuni Mkoa wa Mara umepiga hatua kutoka kuwa mwishoni hadi nafasi ya 17 kitaifa mwaka.

“Kama Mkoa tumedhamiria kuboresha utekelezaji katika upande wa lishe na tumefanikiwa sana kutokana na ushirikiano mkubwa tulioupata kutoka kwa wataalamu mbalimbali na viongozi katika Mkoa wa Mara” alisema Dkt. Tinuga.

Viashiria vinavyopimwa ni pamoja na asilimia ya vikao vya Kamati ya Lishe katika ngazi za halmashauri, asilimia ya usimamizi shirikishi, asilimia ya kaguzi za chakula, asilimia ya wamama waliopewa ushauri wa ulishaji na wahudumu wa afya ngazi ya jamii na asilimia ya wamama waliopewa ushauri wa ulishaji na wahudumu wa afya vituoni.

Viashiria vingine ni asilimia ya watoto waliopatiwa matibabu ya utapiamlo; asilimia ya watoto waliopatiwa matone ya vitamin A; asilimia ya madini ya chuma kwa wamama wajawazito; fedha zilizotumika; fedha zilizotengwa na halmashauri.

Aidha katika kikao hicho Mkoa umeadhimia pia kuongeza kiasi cha fedha kinachotengwa na halmashauri za wilaya kwa ajili ya ktumika katika afua mbalimbali za lishe kwa watoto chini ya miaka mitano.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Demokrasia inaendelea kupevuka katika Mkoa wa Mara: Mtambi

    October 16, 2025
  • Biteko aitaka CWT kuendana na kasi ya mabadiliko duniani

    October 16, 2025
  • RC awapokea Maafisa na wanafunzi kutoka Chuo cha Jeshi cha CSC

    October 13, 2025
  • RC awapokea Madaktari Bingwa wa Mama Samia 64 Mara

    October 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa