• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaanza Kuchukua Hatua

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameanza kuchukua hatua mbalimbali katika utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoyatoa katika ziara yake mkoani Mara tarehe 4-7 Februari, 2022.

Akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya miradi kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji Mheshimiwa Hapi ameagiza mamlaka zinazohusika kuwasimamisha kazi watumishi saba kutokana na makosa mbalimbali katika usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Mara. 

“Hawa wamekuwa wanatuhumiwa kuwa na matatizo mbalimbali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mara, sasa wasimamishwe ili kupisha uchunguzi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Watendaji aliyoelekezwa wasimamishwe ni Bi. Mariam Chacha, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi Halmashauri ya Wilaya ya Tarime; Mhandisi Maige James Gibai, Mkuu wa Idara ya Uhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma; Bi. Maria Nyandoro Chokongoye Mhasibu wa Mapato wa Hamashauri ya Wilaya ya Musoma na Bwana Joseph Orest Luhwa maarufu kama Msuya Afisa katika Idara ya Uvuvi katika Manispaa ya Musoma.

Watendaji wengine ni Bwana Leonard Lukawe Mkau Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Bwana Buzana M. Kazare, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Bwana Nzaya Muhoja, Afisa Manunuzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWASA)

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kufuatilia utendaji wa Waganga Wakuu wa Halmashauri za Wilaya za Tarime, Bunda na Musoma, Mweka Hazina wa Manispaa ya Musoma na Afisa Elimu wa Sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Aidha katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa pia amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya za Musoma, Bunda na Tarime kujieleza kwa maandishi kwa nini Halmashauri zao hazikuomba fedha za miradi ya maendeleo iliyotengwa katika bajeti ya mwaka 2021/2022 kwa mujibu wa utaratibu wa fedha za miradi ya maendeleo.

“Tangu tumeanza kutekeleza bajeti ya mwaka huu, huu ni mwezi wa nane sasa tumeanza lakini hawa hawajaomba fedha hizo na miradi hii haijaanza kutekelezwa, wakati wengine wameshaomba na tayari fedha hizo wameshapata na zimeanza kutekeleza miradi iliyopangwa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa fedha hizo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya miradi ya elimu, afya, nyumba za watumishi na ofisi za Halmashauri.

Fedha ambazo hazijaombwa mpaka sasa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ni Tshs. 2,875,000,000/=, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Tshs.2,362,500,000/=, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Tshs. 1,862,5000,000/=.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara kufanya uchunguzi katika mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Watu wenye Ulemavu na Vijana ili kubaini uwepo wa mikopo hewa na kuwasilisha taarifa kwa Mkoa wa Mkoa ndani ya wiki mbili. 

Mheshimiwa Hapi ameitaka Halmashauri na Wilaya ya Bunda kwa kushirikiana na Kamati ya Usalama ya Wilaya kufanya uchambuzi wa maafisa wanaokaimu ambao baadhi yao wanatuhumiwa kuhujumu uchunguzi unaoendelea kufanyika.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa wiki mbili kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha fedha zote za mapato ya ndani ambazo hazijaingizwa benki ziwe zimeingizwa na Wakurugenzi wa Halmashauri wawasilishe wawasilishe majina ya wahusika wote waliokula fedha mbichi na hatua zilizochukuliwa.

“Kwa sasa hivi halmashauri zote zinafedha ambazo zimekusanywa kama mapato ya ndani na hazijaingizwa benki kiasi cha bilioni 1.795 sasa ninataka kupata taarifa ya pesa hizi mbichi zipo kwenye akounti za halmashauri au ni nani aliyekula tushughulike nae” alisema Mheshimiwa Hapi.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, Makatibu Tawala wa Wilaya, Meya wa Manispaa ya Musoma, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Wakuui wa Taasisi, Wakuu wa Polisi wa Wilaya zote za Kipolisi katika Mkoa wa Mara, Makamanda wa TAKUKURU wa Wilaya na Maktibu Tarafa wote wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa