• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaaimarisha udhibiti wa Uvuvi Haramu

Posted on: June 6th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Musoma kwa kununua boti ya doria kwa ajili ya udhibiti wa uvuvi haramu katika Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Malima ametoa pongezi hizo tarehe 4 Juni 2020 wakati akizindua rasmi boti ya kisasa iliyonunuliwa na Manispaa ya Musoma kwa ajili ya kudhibiti uvuvi haramu.

“Mimi ninawapongeza sana Manispaa ya Musoma kwa kuwa Halmashauri ya kwanza katika Mkoa wa Mara kwa kununua boti itakayoongeza nguvu katika mapambano dhidi ya uvuvi haramu katika Ziwa Victoria” alisema Mheshimiwa Malima.

Ameeleza kuwa jitihada mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa na Mkoa wa Mara katika kulinda raslimali za ziwa ikiwemo kudhibiti uvuvi haramu na ununuzi wa boti hiyo ya kisasa utaimarisha zaidi jitihada hizo na matokeo ni kuongezeka kwa samami na mapato yatokanayo na uvuvi.

Mheshimiwa Malima ameitaka Halmashauri hiyo kuitunza boti hiyo ili itumike muda mrefu kwa manufaa ya wananchi wa Manispaa ya Musoma.

Aidha amempongeza sana Mkuu wa Wilaya ya Musoma kwa kuwa mstari wa mbele katika juhudi za kudhibiti uvuvi haramu katika Mkoa wa Mara. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Vincent Naano Anney ameeleza kuwa halmashauri zote mbili za wilaya hiyo zimeongeza sana makusanyo yanayotokana na uvuvi tangia serikali ya awamu ya tano iingie madarakani na hivyo ununuzi wa boti hii unalenga kuimarisha jitihada hizo.

Ameeleza kuwa halmashauri za Manispaa ya Musoma na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma zinapata jumla ya makusanyo ya shilingi 1.2 bilioni kwa mwaka.

“Kabla ya kuimarisha udhibiti, halmashauri zote mbili zilikuwa zinapata kiasi cha shilingi 160,000 tu kwa mwaka na sasa makusanyo yamepanda maradufu” alisema Dkt. Naano.

Boti hiyo ya kisasa inauwezo wa kuchukua abiria nane na inauwezo wa kukimbia zaidi ya boti za awali zilizokuwa zinatumika katika kudhibiti uvuvi haramu na imenunuliwa kwa gharama ya shilingi milioni 39 ikiwa na vifaa vya usalama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa