• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaadhimisha miaka 60 ya Muungano kwa kupanda miti

Posted on: April 23rd, 2024

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Moses Kaegele leo ameongoza zoezi la kupanda miti katika Shule ya Sekondari ya Butiama ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania na kuwataka wananchi kuhifadhi mazingira kwa kupanda miti.

Mhe. Kaegele ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Butiama ametoa rai hiyo wakati wa zoezi la upandaji miti 1000 katika eneo hilo na kuwataka wanafunzi kuwaelimisha wazazi, walezi na jamii kwa ujumla umuhimu wa kupanda miti kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.

“Watu wakipanda miti kwa wingi, watatunza mazingira na kupata faida mbalimbali za kijamii na za kiuchumi ambazo hazitapatikana kama nchi yetu haitakuwa na miti ya kutosha ili kuhifadhi mazingira yetu” amesema Mhe. Kaegele.

Mhe. Kaegele amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wazuri katika kupanda miti na kutunza miti iliyopandwa na kuwa mfano bora katika utunzaji wa mazingira.

Mwakilishi huyo wa Mkuu wa Mkoa ametumia nafasi hiyo kuwaonya watu wote wanaojihusisha na biashara ya mkaa na kuni bila ya kuwa na vibali na leseni zinazohitajika kuendesha biashara hiyo na kuahidi kuwa serikali itawachukulia hatua kali watakaobainika kukiuka sheria, kanuni na taratibu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Maliasili na Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Butiama Bwana Emanuel Makoye ameeleza kuwa utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ni muhimu sana na kama hakuna uhifadhi wa mazingira hakuna maisha.

“Tunapoyatunza mazingira tunajiepusha na athari nyingi kutokea na tunatunza vyanzo vya maji na tunajilinda dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi” amesema Bwana Makoye.

Bwana Makoye ameeleza kuwa kwa kupanda miti jamii inapata manufaa makubwa ya kiuchumi na kijamii na kuwataka wanafunzi kuwa mabalozi wazuri katika utunzaji wa mazingira.

Bwana Makoye ameeleza kuwa katika maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania, jumla ya miti 1000 inategemewa kupandwa katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na misindano, mikongo, mikaratusi na misandawe.   

Kwa Mkoa wa Mara maadhimisho haya yamefanyika katika Halmashauri zote tisa kwa kufanya shughuli za usafi wa mazingira, kupanda miti, michezo na kuwasaidia wahanga wa mafuriko katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

 Maadhimisho ya miaka 60 kitaifa yanategemea kufanyika tarehe 26 Aprili, 2024 katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam yakiwa na kauli mbiu inayosema: Tumeshikamana na Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa letu.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa