• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kuwawezesha wanawake kiuchumi kupunguza ukatili

Posted on: June 30th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Musabila Kusaya Juni 30, 2025 amezindua Mpango Mkakati wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) katika Ukumbi wa Manispaa ya Musoma na kuziagiza Halmashauri kuanzisha mikakati ya kuwawezesha wanawake kiuchumi ili kupunguza matukio ya ukatili kwa wanawake na watoto.  

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la UNFPA na Shirika lisilo la kiserikali la WILDAF, Ndugu Kusaya amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha Mkoa wa Mara unaweka mkazo katika utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake.

“Sisi kama Mkoa lazima tuwe vinara katika kupambana na matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na tutapambana kwa kuwawezesha wanawake kupata mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri pamoja na fursa nyingine za kukuza uchumi wao” amesema Ndugu Kusaya.

Ndugu Kusaya amesema kuwa vikundi vya wanawake katika Mkoa wa Mara vimekuwa vinarejesha kwa wakati mikopo inayotolewa na kuwahakikishia kuwa Serikali itaendelea kuwawezesha ili kuziwezesha familia kiuchumi.

Wakati huo huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara ameziagiza Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kutenga bajeti ya kujenga nyumba salama ili kuwahifadhi watoto wanaopata changamoto za unyanyasaji na hususan kuhusiana na ukeketaji katika maeneo yao kuweza kuhifadhiwa humo.

Aidha, Ndugu Kusaya ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wazazi na walezi wenye watoto wanaosoma shule za msingi na sekondari za kutwa kuchangia chakula shuleni na kuhakikisha watoto wanapata chakula cha mchana shuleni.

“Kwa sasa upatikanaji wa chakula cha mchana kwa wanafunzi wanaosoma shule za  kutwa ni kwa asilimia 54 tu, tunawatesa watoto wetu kwa kushinda na njaa wakiwa shuleni” amesema Ndugu Kusaya.

Awali akizungumza wakati akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mara Bibi Neema Ibamba amesema mkakati huo utakuwa nyenzo ya kufanyia kazi kwa wadau na Serikali katika kupunguza ukatili kwa wanawake na watoto.

Bibi Ibamba amewapongeza washiriki wote walioshiriki katika uzinduzi wa mpango mkakati huo kwa kushiriki shughuli hiyo na kuwataka kusaidia kutoa elimu katika maeneo yao kuhusiana na mkakati huo.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda  Bi. Jesca Msamba amesema amefurahi kuona jitihada za Serikali katika kuendeleza mapambano ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini nzima.

Bi Jesca amesema Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imejipanga kuhakikisha shabaha ya Serikali katika kupunguza ukatili dhidi ya wanawake na watoto inafanikiwa na kuwahikisha kuwa Bunda inakuwa na jamii salama isiyo na ukatili.

Kwa upande wake Mwalimu wa Shule ya Msingi Nyarigamba A, Mwalimu Deogratius Mungure ambaye pia ni mkalimali wa lugha ya alama amesema jamii inahitaji elimu ya kutosha juu ya ukatili wa kijinsia hasa watoto wenye ulemavu kwa kuwa yapo matukio ya ukatili wanayofanyiwa watoto wenye ulemavu ambayo hayaripotiwi.

Uzinduzi wa Mkakati huo umehudhuriwa na Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Halmashauri, viongozi wa taasisi za dini, mashirika yasiyo ya kiserikali na vyama vya siasa.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Mtambi akutana na viongozi wa dini na kuwasistiza kuhamasisha amani

    August 22, 2025
  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa